Kukutana kwa Mara ya Kwanza
Amit alilelewa katika familia ya Uhindu na alishiriki katika taratibu zote za kidini. Akiwa mtoto aliomba kila siku. Alikuwa amedhamiria lakini alisikia utupu wa kiroho. Amit alisoma maandiko ya Kihindu ili kujitahidi kuelewa dini yake vema. Aliambiwa kwamba haijalishi ni Imani gani kwa sababu dini zote zinatupeleka kwa Mungu. Alitaka kutafuta ukweli halisi ambao utamwongoza Yeye kwa Mungu, lakini alijiuliza kama kweli hiyo kweli ipo.
