Search Course
Search through all lessons and sections in this course
Searching...
No results found
No matches for ""
Try different keywords or check your spelling
Kanuni za Kutafsiri Biblia
Course Description
Kozi hii inafundisha kuhusu kanuni na mbinu za kufasiri Biblia ipasavyo ili kuongoza maisha na uhusiano wetu na Mungu.
Introduction
Kozi hii inatoa utangulizi wa kanuni za msingi za kutafsiri Biblia. Masomo mengi katika kozi hii yana msingi katika Kitabu maarufu, Living by the Book, cha Howard na William Hendricks. Endapo unaweza kukipata kitabu hiki, utaweza kupata mazoezi ili kufanyia kazi kanuni zinazofundishwa katika kozi, vile vile utapata majadiliano zaidi katika kila kanuni. Hata hivyo, kitabu hakihitajiki kwa ajili ya kozi. Nyenzo zote zinazohitajika zimejumuishwa katika masomo haya.
Mwanafunzi anatakiwa kusoma kila Somo kabla ya kuja darasani. Unapaswa kupanga kuwa na dakika 90-120 kwa kila kipindi, Pamoja na muda wa mazoezi nje ya darasa. Kwa sababu kozi hii ina msingi katika mazoezi ya vitendo, unaweza kupenda kugawanya somo katika vipindi zaidi ya kimoja. Hii inaweza kuwapa wanafunzi muda zaidi wa kufanya shughuli.
Masomo yanajumuisha shughuli kadhaa kwa ajili ya kutendea kazi kanuni zinazofundishwa katika somo. Ni muhimu kwamba mwanafunzi achukue muda kufanya shughuli hizi kwa umakini. Shughuli hizi zinatembea katika Maandiko mengi tofauti tofauti. Usikimbilie kumaliza somo. Kwa sababu shughuli nyingi kati ya hizi zitakuwa mpya kwa mwanafunzi, chukua muda darasani ili kuhakikisha kwamba kila mwanafunzi anaelewa namna ya kukamilisha shughuli hizi. Lengo la msingi si kupata jawabu fulani; lengo la msingi ni kukuza stadi katika kujifunza na kutafsiri Biblia.
Mwishoni mwa kozi hii, mwanafunzi atakuwa amesoma vifungu kadhaa vya Maandiko. Kila mwanafunzi atunze nakili zake alizoziandika wakati wa kozi katika daftari lake kwa ajili ya matumizi ya baadae. Kazi zilizofanyika katika kozi hii zitakuwa msaada kwa ajili ya kuandaa ujumbe na somo la Biblia.
Maswali ya majadiliano na shughuli za darasani zimeoneshwa kwa dondoo mshale ►. Kwa habari ya maswali ya majadiliano, wanafunzi wajadili majibu. Jaribu kuhakikisha kwamba wanafunzi wote darasani wanahusika katika majadiliano. Kama itabidi, waite wanafunzi kwa majina yao.
Kila mwanafunzi atafanyia kazi mradi wa kozi katika kipindi chote cha kozi. Baada ya Somo la 10, watawasilisha darasani au watakusanya kazi zao kwa kiongozi wa darasa. Maelekezo kwa ajili ya mawasilisho au kazi yametolewa katika sehemu ya Mazoezi ya Somo la 10.
Mazoezi mengine kadaa pia yamejumuishwa mwishoni mwa Somo la 2 na 7. Wanafunzi wamuoneshe kiongozi wa darasa kazi zilizokamilika lakini watunze nakala ya kazi zao katika shajala zao.
Ready to Start Learning?
Choose a lesson to begin your journey through this course.
Course Lessons
Print Course
SGC exists to equip rising Christian leaders around the world by providing free, high-quality theological resources. We gladly grant permission for you to print and distribute our courses under these simple guidelines:
- No Changes – Course content must not be altered in any way.
- No Profit Sales – Printed copies may not be sold for profit.
- Free Use for Ministry – Churches, schools, and other training ministries may freely print and distribute copies—even if they charge tuition.
- No Unauthorized Translations – Please contact us before translating any course into another language.
All materials remain the copyrighted property of Shepherds Global Classroom. We simply ask that you honor the integrity of the content and mission.
Questions? Reach out to us anytime at info@shepherdsglobal.org
Order Physical Course
Kanuni za Kutafsiri Biblia
Total
$21.99Download Course
By submitting your contact info, you agree to receive occasional email updates about this ministry.
Additional Files
Audio Course Downloads
Kanuni za Kutafsiri Biblia
Download audio files for offline listening
No audio files are available for this course yet.
Check back soon or visit our audio courses page.
Share This Course
Kanuni za Kutafsiri Biblia
Share this free course with others