Type at least 2 characters to search
No results found for ""
Courses
Lessons
navigate open
See all results →

Lesson

Playlist

Mapitio ya Agano Jipya

Mapitio ya Agano Jipya

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Mapitio ya Agano Jipya

Lead Writer: Randall McElwain

Course Description

Kozi hii inafundisha kuhusu maudhui na mafundisho ya msingi ya vitabu 27 vya Agano Jipya.

What You'll Learn

Utangulizi wa Agano Jipya
Mathayo, Marko, na Luka: Maisha ya Kristo
Yohana: Injili ya Kuamini
Matendo ya Mitume: Kanisa la Kwanza
Warumi: Haki ya Mungu
Wakorintho na Wagalatia: Barua kwa Makanisa Yenye Shida
Waefeso, Wafilipi, Wakolosai, na Filemoni: Nyaraka Kutoka Gerezani
Wathesalonike: Kurudi kwa Kristo
Timotheo na Tito: Nyaraka kwa Wachungaji
Waebrania na Yakobo: Nyaraka za Watu Wote, Sehemu ya 1
Petro, Yohana, na Yuda: Nyaraka za Watu Wote, Sehemu ya 2
Ufunuo: Yesu ni Bwana

Course Objectives

Malengo yameorodheshwa mwanzoni mwa kila somo.

Introduction

Kabla ya kukutana kwa ajili ya kila kipindi cha darasa, wanafunzi wasome au wasikilize kitabu (vitabu) vya Biblia ambavyo watajifunza. Mwishoni mwa kila kipindi cha darasa, tafadhali wakumbushe wanafunzi kuhusu zoezi la kusoma kwa ajili ya somo linalofuata. Usomaji huu utahakikisha kwamba wanafumzi wanakuwa na uelewa wa yaliyomo ambayo ni ya msingi kwa kitabu (vitabu) kabla ya darasa kuanza.

Mnapojifunza kama darasa, mnaweza kupokezana kusoma makala. Mara kwa mara mnatakiwa kutulia kidogo kwa ajili ya majadiliano. Kama kiongozi wa darasa, unawajibika kwa ajili ya kuhakikisha majadiliano yanalenga makala zinazosomwa. Itasaidia sana kuwa na kipimo cha muda kwa kila kipindi cha majadiliano.

Maswali ya majadiliano na shughuli za ndani ya darasa yameoneshwa kwa alama ►. Unapaswa kuuliza swali na kuwapa wanafunzi muda wa kujadili majibu yao. Jaribu kuwahusisha wanafunzi wote katika majadiliano. Kama itahitajika, unaweza kuwataja wanafunzi kwa majina yao.

Rejea nyingi za Maandiko zimetolewa katika maandishi. Wanafunzi wanapaswa kutumia Biblia zao wakati wa darasa, ili kuangalia vifungu vinavyojadiliwa.

Kila somo litahusisha jaribio na angalau mradi au zoezi la kuandika ambalo linahusiana na kitabu (vitabu) na dhana kuu zinazojadiliwa katika somo.

Mwishoni mwa kila kipindi, unaweza ukapitia tena maswali ya jaribio pamoja na wanafunzi. Kipindi cha darasa kinachofuata kinapaswa kuanza na jaribio. Jaribio linaweza kufanyika kwa mdomo au kwa maandishi. Kila mwanafunzi anapaswa ajibu maswali kwa kujitegemea (peke yake), pasipo msaada kutoka kwa wengine au pasipo kutumia nyenzo zilizoandikwa. Angalau majibu ya majaribio yanapatikana kwa kuyapakua kutoka katika shepherdsglobal.org.

Kila somo litaanza na zoezi fupi la kukariri andiko, ambalo litahusisha mstari mkuu kutoka katika vitabu vinavyosomwa. Wanafunzi wanategemewa kuandika au kunukuu kifungu cha maandiko kutoka katika kumbukumbu yao wakati wa majaribio.

Endapo mwanafunzi anataka kupata cheti kutoka Shepherds Global Classroom, anapaswa ahudhurie vipindi vya darasa na kukamilisha mazoezi yote. Fomu itatolewa mwishoni mwa kozi kwa ajili ya kunakili mazoezi yote yaliyokamilika.

Kama unaipata kozi hii kupitia SGC mobile app, tafadhali weka umakini katika vyanzo vifuatavyo ambavyo vinapatikana katika kiambatanisho:

Ready to Start Learning?

Choose a lesson to begin your journey through this course.