Kukutana kwa Mara ya Kwanza
Waligonga mlango wa Samweli na wakampatia nakala ya gazeti la Awake. Wageni walikuwa mwanamke na Watoto wake wawili. Walikuwa wamevaa vizuri na walikua na hali ya urafiki. Andiko la gazeti lilihusu namna ya kuwasaidia Watoto kufanya vizuri shuleni. Mwanamke alisoma mstari katika Biblia, akatoa mafafanuzi juu yake, na kisha akamuuliza Samweli endapo angekuwa na shahuku ya kutembelewa kwa ajili ya kujifunza Biblia. Samweli alisema angefikiria kuhusu hilo.