Type at least 2 characters to search
No results found for ""
Courses
Lessons
navigate open
See all results →
Misingi ya Imani ya Kikristo

Misingi ya Imani ya Kikristo

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 3: Utatu Mtakatifu

25 min read

by Stephen Gibson


Malengo ya Somo

(1) Mwanafunzi atakuwa na uwezo wa kuelezea:

  • Namna Utatu Mtakatifu unajibu swali la “Mungu ni nani?”

  • Namna imani yetu juu ya Utatu Mtakatifu inavyotusaidia sisi kuomba na kumuabudu Mungu kiundani zaidi.

  • Namna Utatu Mtakatifu unavyofunuliwa katika Injili.

  • Mistari mikuu katika Biblia kuhusiana na fundisho la Utatu Mtakatifu.

  • Umuhimu wa maneno mahususi ambayo tunayatumia kuzungumza kuhusiana na Utatu Mtakatifu, na ambayo yanapaswa kutumika.

  • Ni kwa namna gani Utatu Mtakatifu unaelezea mapenzi ya Mungu kwa uumbaji, ukombozi,na kanisa.

  • Tamko la Imani ya Kikristo kuhusiana na Utatu Mtakatifu.

(2) Mwanafunzi atakuwa na uwezo wa kutambua mafundisho potofu au uzushi ambayo yanamuwasilisha Mungu kama aliyegawanyika katika vipande vipande au kwamba kushindwa kutofautisha kati ya Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu.