► Soma Waefeso 3:3-10 kwa pamoja. Kifungu hiki kinatueleza nini kuhusu kanisa?
Katika karne za kwanza za Agano Jipya, kanisa lilikuwa ni siri ambayo haikufunuliwa kikamilifu. Kulikuwa na watu waliopokea neema ya Mungu na kuishi katika uhusiano na Yeye (Warumi 4:1-8), lakini kanisa lilikuwa bado halijaanzishwa.
► Kanisa lilianza lini?
Kanisa lilianza kwa maisha na huduma ya Yesu. Kanisa lilijengwa juu ya wokovu alioutoa (Mathayo 16:16-18). Kipindi cha kanisa kilianza Siku ya Pentekoste. Tangu siku hiyo, kanisa lilifanya kazi kwa nguvu za Roho Mtakatifu, bila uongozi wa kimwili na unaoonekana wa Kristo duniani (Yohana 16:7).
Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kueneza na kuanzisha mafundisho yake ulimwenguni kote (Mathayo 28:18-20) na akaahidi kwamba Roho Mtakatifu angewaongoza katika kweli yote (Yohana 16:13). Kanisa linaweza kuitwa la kitume kwa sababu mafundisho ya mitume ndiyo mafundisho ya msingi ya kanisa. Imani yoyote inayopingana na mafundisho hayo ya msingi haipaswi kuitwa ya Kikristo.
Kanisa lina misingi katika:
1. Huduma ya Yesu
2. Wokovu ambao umetolewa na Kristo
3. Tukio lililotokea siku ya Pentekoste
4. Kuendelea kwa mafundisho ya Mitume
Kanisa kama Taasisi Iliyo Hai
Kanisa linafananishwa na familia ambapo Mungu ni Baba na waamini ni kaka na dada (Mathayo 12:48-50, Wakolosai 1:2). Kanisa linaitwa taifa lisilo na asili ya kikabila au chanzo cha asili (1 Petro 2:9-10). Kanisa linafananishwa na mwili ambao Kristo ni kichwa chake (Waefeso 4:15-16, Waefeso 5:30). Washirika hufanya kazi pamoja na kujaliana (kila mmoja kumjali mwingine) (1 Wakorintho 12:14, 26).
Kama mshirika wa mwili wa Kristo, Mkristo hapaswi kuwa na mtazamo wa kujitegemea pekee tofauti na kanisa. Anawahitaji washirika wengine, na wao wanamuhitaji (1 Wakorintho 12:21). Si sahihi kwa Mkristo kuishi kana kwamba anajitosheleza kiroho pasipo kanisa.
Kujitenga na kanisa ni kujitenga na kile ambacho Kristo anakifanya duniani. Kutoliheshimu na kulipenda kanisa ni kutomheshimu na kutompenda Kristo.
Kanisa kama Mwili wa Kristo, wa Mahali Pamoja
Kuna kanisa moja la ulimwengu mzima/wote, lakini pia lipo kanisa la mahali pamoja. Viungo vya mwili haviwezi kufanya kazi isipokuwa viwe pamoja mahali pamoja. Paulo aliwaandikia waamini wa Korintho kwamba wao ni mwili wa Kristo (1 Wakorintho 12:27), jambo linaloonyesha kwamba kanisa la mahali pamoja ni mwili wa Kristo katika eneo hilo.
Mungu amelitengeneza kanisa la mahali pamoja kuwa familia ya Imani:
1. Linalofanya kazi kama mwili wenye karama za kiroho.
2. Linalokidhi mahitaji mbalimbali ya washirika (kwa rasilimali za kibinadamu na za kimungu).
3. Linalouonesha ulimwengu ulimwengu hekima ya Mungu katika kila eneo la maisha.
4. Linalowaalika wasioamini watubu na kuingia katika familia.
Ushirika wa kweli unajumuisha uchumi kwa sababu wale ambao wapo katika ushirika wanashiriki maisha pamoja na kila mmoja kujali mahitaji ya mwingine (Yakobo 2:15-16, Yakobo 1:27). Mahitaji wa ndugu wa kiume na wa kike katika Kristo ni wajibu wa kanisa endapo mshirika huyo anashiriki katika Maisha ya kanisa na kufanya wajibu wake kwa kadiri inavyowezekana.
Mungu hutoa karama za Kiroho na wito maalumu kwa ajili ya kulijenga na kuliimarisha kanisa la mahali pamoja (Waefeso 4:11-12).
Kanisa la mahali pamoja huihudumia jamii yake. Kipaumbele cha kwanza ni cha kiroho—kuhubiri injili na kuendeleza kweli ya Mungu katika masuala yote. Kanisa pia hushughulikia mahitaji ya kimwili katika jamii, lakini hutoa kipaumbele kwa wale walio katika ushirika wa kiroho wa kanisa (Wagalatia 6:10).
Kutakasa Kanisa
Yesu alijitoa kwa ajili ya kanisa ili kulifanya takatifu na lisilo na doa (Waefeso 5:27). Kanisa halipaswi kamwe kuhalalisha dhambi, ingawa daima linapaswa kuwa tayari kusamehe. Viongozi wanapaswa kuwa mifano ya maisha matakatifu (1 Timotheo 3:2-3). Ikiwa mshirika wa kanisa anatenda dhambi, anapaswa kukemewa na hatimaye kuondolewa katika ushirika endapo hatatubu (1 Wakorintho 5:11-13).
► Kwa nini kanisa si kamilifu?
Watu wa kanisa hawatakuwa wakamilifu kwa kila namna. Kwa sababu kanisa linahubiri injili, kuna watu katika mkusanyiko ambao bado hawajatubu dhambi. Hata miongoni mwa waliookoka, bado kutakuwa na mapungufu kwa sababu hawajaelewa jinsi ya kutumia kweli katika kila eneo la maisha yao. Hata miongoni mwa Wakristo waliokomaa, kunaweza kuwa na mapungufu na mitazamo isiyo sahihi kwa sababu hata Mkristo aliyekomaa bado yuko katika mchakato wa kukua kiroho. Ni sehemu ya kazi ya kanisa kuendelea kufundisha na kutumia Neno la Mungu ili kuwaleta watu katika ukomavu wa kiroho (Waefeso 4:11-16; 2 Timotheo 3:16-17).
Kufafanua Kanisa
Kanisa la Kiulimwengu linajumuisha waamini wote katika nyakati zote na mahali pote. Wakati mwingine linaitwa kanisa lisiloonekana kwa sababu hakuna taasisi ya kidunia ambayo inashughulika katika kulisimamia au lenye orodha ya washiriki wake wote.
Kanisa la Mahali Pamoja ni jamii ya waumini katika eneo moja wanaofanya pamoja kazi ya mwili wa Kristo. Kikundi si kanisa ikiwa kimeundwa kwa kusudi finyu zaidi na zenye mipaka.
Huu ni ufafanuzi mpana Zaidi wa kanisa la mahali pamoja: “Kundi la waamini waliobatizwa [waliounganishwa] pamoja kwa ajili ya ibada, kujengwa kiroho, huduma, ushirika, na uinjilisti; wanaokubali uongozi wa kiroho; walio tayari kuhudumia sehemu zote za jamii kupitia karama mbalimbali katika mwili; na wanaotekeleza mara kwa mara maagizo ya Bwana.”[1]
[1]David Dockery, Southern Baptist Consensus and Renewal: A Biblical, Historical, and Theological Proposal (Nashville: B&H Publishing Group, 2008), 127
Umoja wa Kanisa la Ulimwengu Mzima
Kuna kanisa moja kwa ajili ya wakati na mahali pote. Yesu alisema, “nitalijenga kanisa langu,” (Mathayo 16:18) sio “makanisa.” Mtume Paulo aliandika kwamba Mwili mmoja, na Roho mmoja, na tumaini moja, kama jinsi ambavyo kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja (Waefeso 4:4-6).
Matamko ya Imani ya kanisa la kwanza yalirejelea “Kanisa Katiloko.” Hii haikurejelea Kanisa la Romani Katoliki, bali kanisa la ulimwengu mzima ambalo linajumuisha Wakristo wote.
[1]Umoja wa kanisa la ulimwengu mzima hauko katika kuwa shirika moja chini ya uongozi mmoja ulio katikati. Hilo halitatokea kamwe kabla ya kurudi kwa Kristo. Watu wengine hutamani lingewezekana, lakini inaonekana kuwa halikuwa mapenzi ya Mungu, kwa sababu Yesu aliwakemea wanafunzi walipodhani kwamba mtu hapaswi kufanya huduma nje ya ushirika wao (Luka 9:49-50). Endapo Yesu angependa kuwepo na uongozi mmoja wa kati juu ya kanisa la ulimwengu mzima, angeweza kubaki duniani kimwili ili kuliongoza. Hata hivyo, Yesu aliona kwamba kazi mbalimbali za Roho Mtakatifu duniani kote zisingetendeka ipasavyo endapo angebaki kimwili duniani (Yohana 16:7).
► Umoja wa Kanisa la Ulimwengu mzima umejengwa katika nini?
Umoja wa kanisa la ulimwengu mzima umejengwa juu ya
1. Mafundisho ya Mitume
2. Uhusiano na Kristo unaobadilisha
Umoja wa mafundisho haumaanishi kwamba Wakristo wanakubaliana katika kila kitu, hata katika mafundisho yote muhimu. Inamaanisha kwamba wanashiriki mafundisho muhimu kuhusiana na asili ya Mungu na Kristo na mambo muhimu ya Injili. Pasipo hayo, hawangeweza kuwa wanamuabudu Mungu mmoja au kupata uzoefu wa neema yake.
[2]Mafundisho sio kitu pekee kinachohitajika katika umoja wa Kikristo. Wakristo wanashiriki muungano wa mahusiano baina yao kwa sababu ya mahusiano yao yanayobadilisha pamoja na Kristo. Kwa sababu wametubu dhambi zao, wameweka Imani yao kwa Kristo na wana Roho Mtakatifu, wana mahusiano maalumu sana. Wakristo wanatambuana duniani kote pasipo kujali tofauti zao katika namna nyingi.
“Endapo moyo wako uko sahihi, kama wangu ulivyo pamoja na moyo wako, basi nipende kwa upendo wa ndani sana, kama rafiki aliye karibu zaidi ya ndugu; kama ndugu katika Kristo, raia mwenzangu wa Yerusalem mpya, askari mwenza anayehusika katika vita ile ile, chini ya kapteni (shujaa) mmoja wa wokovu wetu. Nipende kama mwenzako katika ufalme tukidumu katika kumngoja Yesu, na kuungana naye katika utukufu wake.”
- John Wesley, imefupishwa kutoka mahubiri yake “roho ya katoliki”
“Nimekuja kuamini kwamba alama ya moyo ulitakaswa kiukweli ni kwamba unajali zaidi kuhusu wokovu wa mwingine kuliko kujali kuhusiana na ushwari binafsi.”
– Dennis Kinlaw
Umoja wa Kanisa la Mahali Pamoja
Tunaweza kumkubali kama Mkristo mtu yeyote ambaye ameshikilia mafundisho ya msingi na ya muhimu ya Kikristo na anaye onekana kuwa katika mahusiano yanayobadilisha pamoja na Yesu. Lakini makubaliano ya mafundisho ya kanisa la mahali pamoja lazima yawe ya ndani zaidi.
Kanisa la mahali pamoja ni kundi la watu ambao wamejitoa na wamejikita ili kuabudu pamoja, kushuhudia/kufanya uinjilisti, kufundisha waongofu wapya na Vijana, kutumikia jamii, na kufundisha kwa undani Maisha ya Kikristo. Kwa watu kukamilisha kusudi hilo pamoja, wanapaswa kukubaliana juu ya mambo mengi kuhusiana na mafundisho.
Kwa mfano, pengine mtu katika kanisa la mahali pamoja anamwambia kila kijana na mwongofu mpya kuomba karama ya kunena kwa lugha. Lakini viongozi wengine katika kanisa hilo hawaamini kwamba zawadi ya kunena kwa lugha imeahidiwa kwa kila mwamini. Wana wasiwasi kwamba watu wataingia katika machafuko ya Kiroho endapo watajaribu kupata uzoefu wa jambo ambalo si mapenzi ya Mungu. Ni wazi kwamba, itakuwa ngumu kwa watu hawa kufanya kazi kwa pamoja katika kanisa la mahali pamoja. Hata kama viongozi watamchukulia mtu huyu kama mwamini, hawatamruhusu kufundisha mafundisho ambayo yanaweza kuleta machafuko katika kusanyiko hilo.
Kanisa la mahali pamoja linahitaji kukubaliana juu ya mfundisho ambayo yataathiri namna ambavyo wanashiriki maisha pamoja na kufanya huduma. Ni nzuri/vema kwa kanisa kuwa na tamko lililoandikwa la mafundisho ambayo wanashiriki. Tamko halitatumika kuamua endapo mtu ni mwamini. Badala yake, litaonesha ni mafundisho yapi yanawaunganisha waamini kwa ukaribu zaidi na katika ibada za kawaida na huduma.
Sakramenti za Kanisa
Yesu alitoa sakramenti kwa kanisa. Zinaweza pia kuitwa taratibu za kanisa au sherehe za kanisa.
Ubatizo ni alama ya kifo cha Yesu na ufufuo (Warumi 6:3-4). Ubatizo ni ushuhuda kwamba mwamini amejifananisha na Kristo na amepata uzoefu wa kifo cha dhambi na maisha mapya katika Kristo. Ubatizo haumuokoi mtu. Ubatizo ni ushuhuda wa hadharani kwamba mabadiliko yametokea (Yohana 3:7-8).
Meza ya Bwana ilianzishwa na Yesu katika chakula chake cha mwisho akiwa pamoja na wanafunzi wake kabla ya kuteswa (1 Wakorintho 11:23-25). Mkate na divai ni uwakilishi wa damu na mwili wa Kristo uliotolewa kama sadaka kwa ajili ya wokovu wetu.[1] Kama ambavyo tunakula chakula cha kimwili, tunategemea sana sadaka yake kwa ajili ya maisha ya Kiroho (Yohana 6:53-58).
Sakramenti zinaweza kuitwa “njia za neema.” Hazileti au hazitoi neema endapo zitafanya pasipo Imani na utii. Ni mazoezi ambayo Mungu ameyatoa kwetu, na endapo yatafanyika katika Imani, ni njia ya sisi kupata neema kutoka kwa Mungu.
► Nini ni baadhi ya makusudi ya kanisa?
[1]Picha: "The Lord's Supper" ilipigwa na Allison Estabrook tarehe Oct. 14, 2022, ilichukuliwa tena kutoka https://www.flickr.com/photos/sgc-library/52476662295/, leseni chini ya CC BY 4.0.
Baadhi ya Makusudi ya Kanisa la Mahali Yanayopatikana katika Agano Jipya
8. Kutekeleza ubatizo na Meza ya Bwana (Mathayo 28:19; 1 Wakorintho 11:23-26)
9. Kufundisha waumini ili wakomae (Waefeso 4:12-13)
10. Kuhudumia mahitaji ya jamii (Wagalatia 6:10; Waefeso 4:28; Waebrania 13:16)
Nyingi katika hizi haziwezi kufanya na mtu binafsi kwa kujitegemea. Makusudi haya yanategemea ushirikiano ambao unafanywa na kundi la waamini pamoja na uongozi uliopangwa vizuri.
Mungu anamwita kila muumini ajitoe kwa kanisa la mahali pamoja na kulisaidia kanisa kutimiza kusudi lake ulimwenguni. Kanisa halitaweza kutimiliza kusudi lake endapo washirika wa kanisa hawatatimiza wajibu wao kama washirika wa mwili wa Kristo.
“Siamini kwamba Mungu anataka kanisa letu kujikita katika majengo na huduma za kiibada. Badala yake, Mungu anataka makanisa yetu—katika mfumo wowote wa mahususi wa makusanyiko yetu—ujikite katika utume hai wa kufanya wanafunzi, umisheni, na kufuatilia umoja.”
–Francis Chan
Kosa la Kuepuka: Ubinafsi wa Kiroho
Angalizo kwa kiongozi wa darasa: Mshiriki wa darasa anaweza kuelezea sehemu hii.
Baadhi ya watu hawajajikita kuwa sehemu ya kanisa la mahali pamoja. Wanataka kujisikia huru kuhudhiria kanisa lolote siku ya Jumapili. Hawawezi kusaidia huduma yeyote ya kanisa kwa sababu kanisal haliwezi kuwategemea. Hawana mahusiano ambayo yanaruhusu ushirika wa Kiroho na uwajibikaji. Endapo Wakristo wote wakifanya hivyo, hakutakuwa na makanisa.
► Someni Tamko la Imani kwa pamoja angalau mara mbili.
Tamko la Imani
Kristo amelijenga kanisa moja takatifu, la kiulimwengu, linaloonekana kuwa mwili wa Kristo katika makusanyiko ya mahali pamoja. Kanisa linaendelea kushikilia mafundisho ya mitume na kuitetea kweli yote. Kanisa ni familia ya Mungu, yenye ushirika unaohudumia mahitaji yote. Kanisa linamwabudu Mungu, linauhubiri ulimwengu, na kuwafanya waamini kuwa wanafunzi.
Somo la 12 Mazoezi
(1) Zoezi la Kifungu: Kila mwanafunzi atapewa mojawapo ya vifungu vilivyoorodheshwa hapa chini. Kabla ya kipindi kinachofuata cha darasa, unapaswa kusoma kifungu na kuandika aya kuhusiana na somo la somo hili.
1 Wakorintho 5:1-13
1 Wakorintho 6:1-8
1 Wakorintho 12:14-31
Waefeso 4:11-16
Yakobo 2:1-9
(2) Jaribio: Utaanza kipindi kijacho cha darasa kwa jaribio juu la Somo 13. Jifunze kwa umakini maswali wakati wa maandalizi.
(3) Zoezi la Kufundisha: Kumbuka kupanga na kuripoti muda wako wa kufundisha nje ya darasa.
Somo la 12 Jaribio
(1) Kipindi cha kanisa kilianza lini?
(2) Kwa nini kanisa kinaweza kuitwa ka Mitume?
(3) Ni nyanja gani nne za chanzo cha kanisa?
(4) Nani ni kanisa la kiulimwengu?
(5) Kanisa la mahali pamoja ni nini?
(6) Neno Kanisa Katoliko kwa sili linamaanisha nini?
(7) Kanisa la kiulimwengu limeungana katika mambo gani mawili?
(8) Kwa nini ni vizuri kwa kanisa kuwa na tamko la Imani mafundisho ambayo wanashiriki?
(9) Orodhesha makusudi sita ya kanisa la mahali pamoja.
Free to print for ministry use. No changes to content, no profit sales.
SGC exists to equip rising Christian leaders around the world by providing free, high-quality theological resources. We gladly grant permission for you to print and distribute our courses under these simple guidelines:
No Changes – Course content must not be altered in any way.
No Profit Sales – Printed copies may not be sold for profit.
Free Use for Ministry – Churches, schools, and other training ministries may freely print and distribute copies—even if they charge tuition.
No Unauthorized Translations – Please contact us before translating any course into another language.
All materials remain the copyrighted property of Shepherds Global Classroom.