Kifungu cha kujifunza – Warumi Sehemu 5, kifungu cha 2-3
Warumi 10 ni kilele cha kitabu cha Warumi. Mtume tayari alishaeleza kwamba wokovu ni kwa neema kwa njia ya imani na kwamba kila mtu katika ulimwengu huu anauhitaji. Kwa kuwa imani ni ya lazima, ujumbe wa injili ni muhimu: Watu wanahitaji kusikia ujumbe ili kwamba waweze kuuamini. Sura hii ni ya muhimu katika kusudi la kitabu kwa sababu kitabu chote kinatoa msingi wa kazi ya umishenari.
Warumi 11 inahusika na mahusiano kati ya Waisraeli na Kanisa. Wayahudi wengi waliikataa injili. Paulo alielezea kwamba mpango wa Mungu ulikuwa ni dunia yote pamoja na Wayahudi waweze kuokolewa. Waisraeli kwa ujumla wao kuna siku moja watakayomkubali Kristo.