Warumi
Warumi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 5: Njia na Maana ya Kuhesabiwa Haki

18 min read

by Stephen Gibson


Kutoa maana ya Imani Inayookoa

► Je, imani inayookoa ni nini? Kama mtu atakuwa anayo imani inayookoa, hiyo inamaanisha kwamba ameamini nini?

Je, mtu aliyeamini anaamini nini?

(1) Anaamini kwamba hawezi kufanya lolote katika kujihesabia haki mwenyewe.

"Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu" (Waefeso 2:8-9).

Anatambua kwamba hawezi kufanya lolote (matendo) litakalomfanya astahili kuokoka, hata kwa sehemu kidogo tu.

(2) Anaamini kwamba dhabihu ya Kristo inatosha kwa ajili ya msamaha wake.

" Naye ndiye kipatanisho kwa ajili ya dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote" (1 Yohane 2:2).

Kipatanisho inamaanisha ni dhabihu inayofanya msamaha wetu uwezekane.

(3) Anaamini kwamba Mungu atamsamehe yeye kwa sharti la imani peke yake.

"Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote" (1 Yohane 1:9).

Kama anafikiria kwamba kuna masharti mengine, anategemea kuokoka kwa matendo badala ya kuokoka kabisa kwa neema.