Kifungu cha kujifunza – Warumi Sehemu ya 5
Barua kwa Warumi inalezea jinsi mtu anavyoingia katika uhusiano na Mungu ili kupokea wokovu na baraka. Uhusiano na Mungu umejikita katika neema inayopokelewa kwa Imani. Kifugu hiki kinasababisha maswali yanayohusu Israeli. Kunatokea nini katika uhusiano maalumu kati ya Mungu na Israeli? Je, Myahudi nawezaje kuokoka? Je, Mungu bado ana mpango kwa Waisraeli? Sura hizi zinajibu maswali hayo Paulo anapoendelea kuelezea ujumbe wa injili.