Warumi
Warumi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 3: Kosa la Waisraeli

14 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi wa Maandiko yahusuyo siku za mwisho (Apocalyptic)

Maandiko yanayohusu siku za mwisho yanahusu kutunza imani badala ya kulemewa na uovu na kutotenda haki katika dunia wakati wa siku za mwisho. Yanaelezea muda ambao Mungu kwa ghafla ataingilia kati duniani, akiadhibu uovu na akiwasaidia watu wake.[1]

Neno ambalo mara kwa mara linatumika kwa ajili ya muda wa mwisho wa Mungu kuingilia kati ni Siku ya Bwana. Baadhi ya vifungu kwenye Agano la Kale huelezea siku ya Bwana kama ni ule muda ambao Wamataifa wataadhibiwa kwa yale waliyokuwa wameifanyia Israeli.[2] Wayahudi wengi walianza kudhania kwamba Wayahudi hawakuwa na haja ya kuhofia chochote kuhusiana na hukumu ya Mungu. Manabii walijitahidi kuwaonesha kwamba hata wao watapaswa kuhukumiwa kama watakuwa watenda dhambi. (Zefania 1:12, Amosi 5:18-27) na kwamba hawataepuka kwa sababu wao ni Wayahudi; lakini dhana hii iliendelea kubaki.

Ilikuwa ni vigumu kwa Wayahudi kukubali ukweli kwamba walihitaji kuokoka. Kwa mfano, ubatizo ulikuwa ni sherehe waliyoitumia kuwaingiza Wamataifa kwenye Uyahudi. Hawakuwabatiza Wayahudi. Yohane Mbatizaji aliwabatiza Wayahudi, na kitendo chake hicho kiliwaghadhibisha Wayahudi ambao walifikiri kwamba hawakuwa wanahitaji ubatizo au msamaha. Walidhania kwamba walikuwa wamependelewa na Mungu kwa sababu walikuwa ni uzao au watoto wa Ibrahimu (Mathayo 3:9).

Kwenye kitabu cha Warumi, Paulo anarejelea kwenye maneno haya ya “siku ile ya hasira” (2:5) na “katika siku ile Mungu atakapozihukumu” (2:16). Marejeo haya yanatokana na mada iliyoko katika 1:16-18, kwamba injili huleta wokovu unaotuepusha na siku ile ya hasira. Katika 2:2-3 anawashangaza Wayahudi wanaojihesabia haki ambapo ukweli ni kwamba walikuwa pia na sababu ya kuwa na hofu na siku ile ya Bwana. Kwani hata Wayahudi wanahitaji wokovu.


[1]Maandiko ya siku za mwisho katika Agano la Kale ni pamoja na kitabu cha Danieli, Zekaria, Yoeli, Ezekieli 37-39, na Isaya 24-27. Kwenye Agano Jipya, tunapata kitabu cha Mathayo 24, Luka 21, Marko 13, 2 Wathesalonike 2, na Ufunuo.
[2]Baadhi ya mifano ni Zekaria 12 na Yoeli 3.