Kanisa la Rumi
Jiji la Rumi
Wakati ule wa Paulo, jiji la Rumi ndilo lililokuwa kubwa kuliko yote duniani, likiwa na wakazi zaidi ya milioni moja.[1] Kulikuwa na mchanganyiko wa makundi mbalimbali ya kikabila, lugha, na dini. Wengi wa watu walikuwa ni watumwa.
Wamisionari wa kwanza katika Rumi
Hatuwezi kujua ni mtu gani aliyekuwa wa kwanza kupeleka injili katika Rumi. Kwenye siku ya Pentekoste, Wayahudi walikuwepo kutokea Rumi (Matendo 2:10). Wale waliokuwa wamebadilishwa na au kuokoka kwa hakika walichukua ujumbe wa injili wakati wa kurejea Rumi. Tangazo lao kwamba Masihi alishakuja lilisababisha mshangao na utata. Injili iliisambaa kwa haraka miongoni mwa Wamataifa ambao tayari walikuwa wanaiheshimu dini ya Kiyahudi.
Kanisa la Wamataifa
Ingawaje Wayahudi wanatamkwa kwenye sehemu za barua hii, kanisa lililokuwa Rumi lilikuwa na wingi wa watu wamataifa. Paulo aliwaita wamataifa (1:13-15) na akasema kwamba kwa sababu alikuwa ni mdeni kwa Wayunani na watu wote waliojulikana kama washenzi, alikuwa tayari kuhubiri kwa Warumi. Hata hivyo, ushawishi wa Kiyahudi katika kanisa la Rumi ulikuwa wenye nguvu sana, kwa kuwa waamini wa kwanza katika eneo hilo walikuwa ni Wayahudi. Inawezekana kwamba injili ilikuwa bado haijaelezwa kwa ufasaha katika njia ambayo ingewaonesha waamini uhuru wao wa kutoka katika sheria za Kiyahudi.