Warumi
Warumi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 11: Huduma na Mahusiano

17 min read

by Stephen Gibson


Kifungu cha kujifunza – Warumi Sehemu ya 6

Sehemu ya 6 ya Warumi (12:1–15:7) ina maelekezo mengi ya vitendo kwa ajili ya maisha ya kanisa, huduma, mahusiano ya Kikristo, na mahusiano na serikali.

12:1-2 inatambulisha sehemu ya 6, ikituambia kwamba tunapaswa kujitoa kabisa kutumika kwa ajili ya Mungu. Hii inafuatia kutoka maelezo ya Paulo katika sura iliopita: Kwamba tuna deni kwa kila kitu kwa Mungu (11:35), na kwamba njia za Mungu ni za hekima kabisa (11:33).

Paulo anatumia mfano wa dhabihu iliyo hai (12:1). tumejitolea kabisa kama dhabihu inayopaswa kuuawa, lakini badala ya kufa, tunaishi kwa ajili ya Mungu. Hiyo ina maana kwamba msimamo huo ni lazima uzingatiwe. Siku hadi siku ni lazima tukatae kuondoka katika uaminifu wetu. Mfano wa dhabihu iliyo hai unasisitiza kujitoa kwetu kabisa kama sadaka. Hatuwezi tukahifadhi sehemu ya maisha yetu kwa ajili yetu wenyewe nje ya mapenzi ya Mungu. Hatuwezi kulinda baadhi ya matamanio au matarajio kutokana na madai ya kujitolea kabisa kwa Mungu.

Kujitolea huku binafsi kama dhabihu iliyo hai ni ibada ya kiroho, tofauti na mapokeo tu ya dini.[1]

Huduma ya kujitolea kabisa haitawezekana bila ya kuwepo na mabadiliko yaliyoelezwa katika 12:2. Ni lazima tubadilishwe kwa kufanywa upya nia zetu. Hatupaswi kuifuatisha dunia hii katika maadili yake, tabia zake, au maoni yake. Mtu anayetafakari kila swali katika mustakabali wa mapenzi makamilifu ya Mungu atatofautiana na dunia. Hatatoa ruhusa kwa matamanio yeyote ya dhambi; hawezi akayavumilia kana kwamba ni mambo ya kawaida tu.

Tambua kwamba mwili unapaswa uwe mtakatifu. Dhambi siyo kipengele muhimu cha mwili ambacho hakiwezi kutakaswa na Mungu. Mwili siyo wenye kuwa na dhambi wenyewe na hauwezi kutenda dhambi pasipokuwa na mapenzi binafsi ya kufanya hivyo lakini unaweza kutumiwa katika kutenda dhambi.

Aya za kutoka 12:1-15:7 zinaelezea jinsi ya kuishi maisha ya kujitolea kabisa na yaliyobadilishwa.

► Mwanafunzi atapaswa kusoma Warumi 12 kwa ajili ya kikundi.


[1]Ona maelezo ya kumbukumbu yaliyoko katika Warumi 1:9.