Warumi
Warumi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 4: Hali ya Ulimwengu Wote

14 min read

by Stephen Gibson


Neema iletayo Wokovu

Hata kama itatolewa dhabihu, mwenye dhambi hawezi kuwa na matumaini bila ya neema ya Mungu kuwa inafanya kazi ndani ya moyo wake. Mwenye dhambi huwa amekufa kiroho katika dhambi yake, akiwa anatawaliwa na tamaa mbaya, na akiwa chini ya utawala wa shetani. (Wafeso 2:1-3). Hana uwezo wowote wa kubadilisha mwenendo wake (Warumi 7:18-19). Je, ni kwa jinsi gani anaweza kukubaliana na injili kwa toba na imani?

Wanateolojia wamejaribu kuelezea jinsi neema ya Mungu inavyotenda kazi kwenye hali ya uenye dhambi ya mwanadamu.

John Calvin

John Calvin aliamini kwamba kwa sababu mwanadamu amepotoka au amekengeuka kabisa hawezi akawa na chaguo la kuwajibika kwa Mungu.[1] Kwa hiyo, Mungu ndiye anayechagua ni nani atakayeokoka na ni nani ambaye hataokoka. Kwa kuwa Mungu huchagua watu wachache tu kwa ajili ya kuokoka, upatanisho unatolewa kwa ajili yao peke yao na siyo kwa watu wote. Watu hawa hawawezi kuchagua. Kwa neema ambayo haiwezi kuzuiliwa, Mungu huwafanya waweze kutubu na kuamini. Kamwe hawawezi wakaanguka na kutoka kwenye wokovu kwa sababu mapenzi yao yako chini ya uongozi wa Mungu. Hii ilikuwa ni dhana ya John Calvin kuhusiana na mamlaka aliyo nayo Mungu.

Calvin hakuamini kwamba neema iokoayo inapatikana kwa ajili ya kila mtu. Aliamini kwamba hakuna mtu yeyote anayeweza kutubu na kuamini bila ya neema maalumu, na aliamini kwamba neema hiyo haikutolewa kwa watu walio wengi.

Calvin aliamini kwamba mtu hawezi akafanya jambo lolote zuri, kama vile kutunza ahadi, kuipenda familia yake, bila ya kupata msaada wa Mungu. Aliamini kwamba Mungu huwapa watu wote neema inayowawezesha kufanya mambo mazuri. Anaiita neema hii “neema ya kawaida.” Hakuamini kwamba neema ya kawaida inaweza kumpeleka mtu kwenye kuokoka.

John Wesley alikuwa na mtazamo tofauti kuhusiana na neema ya Mungu. Aliona kwamba Biblia kwa mara zote inawaita watu kuwajibika kwa Mungu. Kwa sababu ya hiyo, aliamini kwamba mwanadamu ana uweza wa kuchagua. Aliamini kama Calvin kwamba mwanadamu amepotoka na hawezi kupokea injili bila ya msaada wa Mungu, lakini aliamini kwamba Mungu hutoa huo msaada kwa kila mtu. Aliamini kwamba Mungu huwapa watu nia na uwezo wa kuwajibika, lakini hawalazimishi kuokolewa. Mungu hufanya chaguo la mwanadamu liwe kitu kinachowezekana. Hii ni neema ya mwanzo inayokuja kwa kila mtu. Wanateolojia wameiita “neema ya awali,” ikimaanisha kwamba ni ”neema inayokuja kabla.”

Neema ya Mungu huingia hadi ndani ya moyo wa mwenye dhambi, ikimhukumu kutokana na dhambi zake na ikimwonyesha kwamba yeye mwenyewe ajilaumu kwa kutengana kwake na Mungu. Neema ya Mungu husababisha awe na nia ya msamaha na anampa uwezo wa kumwitikia Mungu.

Bila ya neema, mwenye dhambi hawezi hata kuja kwa Mungu. Neema ya Mungu huja kwa kila mtu kabla hajaanza kumtafuta Mungu, ingawaje huwa hajafanya lolote ili aweze kustahili.

Kumbuka katika Waefeso 2:1-3, je, inatoa maelezo gani yasiyokuwa na matumaini? Lakini angalia aya mbili zinazofuata baada ya maelezo hayo.

Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; (yaani, tumeokolewa kwa neema) (Waefeso 2:4-5).

Kama mtu akiwa hajaokoka, siyo kwa sababu hakuwa na neema, bali ni kwa sababu hakutaka kuwajibikia neema aliyokuwa nayo.

► Je, ni kipi kinachotangulia kwanza, mwanadamu kumtafuta Mungu au kazi ya Mungu ndani ya mwanadamu? Ni kwa jinsi gani utaielezea hii?


[1]Picha: “Portretten van Johannes Calvijn...”, kutoka Rijksmuseum, imepatikana kutoka https://commons.wikimedia.org/wiki/index.php?curid=85920383, mali ya umma.