Warumi
Warumi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 8: Maisha katika Roho

14 min read

by Stephen Gibson


Kifungu cha kujifunza – Warumi Sehemu ya 4, Kifungu cha 3

Katika somo hili tunaendelea na Sehemu ya 4 ya Kitabu cha Warumi. Tumejifunza Warumi 6, kuhusu “ushindi dhidi ya dhambi,” na Warumi 7, kuhusu “mtenda dhambi mwenye hatia.” Katika somo hili tutajifunza Warumi 8, ambayo inaelezea maisha ya Mkristo kwenye hali ngumu za dunia.

Jambo Kuu katika Warumi 8

Ingawaje mwamini anaishi kwenye dunia iliyoanguka, akipata mateso kutokana na hali ya dunia na kutokana na udhaifu wake mwenyewe, Roho Mtakatifu humpa ushindi juu ya dhambi na katika hali zote anazopitia.

Muhtasari wa Warumi Sura ya 8

Sura hii inarejea mara nyingi katika nafsi tatu zilizoko kwenye Utatu Mtakatifu wa Mungu. Nafsi hizi zote tatu zinahusiana kwa karibu sana katika wokovu wetu wa sasa na wa baadaye. Tunaweza kuishi kwa ushindi tukiwa katika hali ya mwili, tunaweza kufurahia kwa uhakika wokovu wetu binafsi, tunaweza kuhimili hali mbalimbali za maanguko zilizopo, tunaweza kuomba kwa msaada wa kiroho zaidi ya akili zetu wenyewe, na tukaendelea kudumu katika uhusiano wetu wa wokovu na Mungu.

8:1-13 zinaunda kifungu ambacho kinaweza kikaitwa “Siyo katika Mwili tena.”

Utangulizi wa Warumi 8:1-13

Wale watu wote ambao hawahukumiwi ni wale ambao hawafuati tena mambo ya mwili. Kuwa katika hali ya kimwili haimaanishi ni kuwa mwanadamu; bali inamaanisha ni kuwa chini ya mamlaka ya hali ya asili ya anguko la dhambi.[1]

Kuwa katika hali ya kimwili inatofautisha na kuwa katika hali ya kuokoka. Hali ya kimwili ni kifo (8:6) na ni uadui na Mungu (8:7). Mtu aliyeko katika hali ya kimwili hawezi akampendeza Mungu (8:8) na lazima atakufa (8:13). Kuwa katika hali ya kimwili ni hali moja inayofanana na ile iliyoelezwa katika 7:7-25 (ona 7:14, 18, 25).

8:12-13 ni hitimisho. Hatupaswi tuishi katika hali ya kimwili, kwa kuwa mtu anayeishi katika hali ya kimwili atakufa, hii ikiwa na maana kwamba ni kupokea hukumu ya Mungu (ona 1:17). Ni lazima tuue matendo ya dhambi ya mwili. Kwa kuwa mtu anayefuata matendo ya kimwili ni mwenye dhambi, sio mfuasi wa Yesu, dhambi ni lazima isambaratishwe kabisa kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

► Mwanafunzi atapaswa kusoma Warumi 8:1-13 kwa ajili ya kikundi.


[1]Mwangalizo katika somo la 7 kuhusu “Kufafanua Mwili/Nyama” ni muhimu sana katika kukielewa kifungu hiki.