Huduma Ya Uongozi
Huduma Ya Uongozi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 2: Sifa za Kibiblia kwa ajili Viongozi

12 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

Baadhi ya watu wanaamini kwamba kwa kuwa wote tuna hadhi moja inayofanana mbele za Mungu, hakupaswi kuwepo na mtu yeyote mwenye mamlaka juu ya wengine katika kanisa. Watu wengi wanasema wanaamini katika uongozi, lakini wanafanya au wanatenda kana kwamba wao ni watu walio huru kutoka katika mamlaka yeyote ya kiroho.

► Je, Biblia inafundisha kwamba inapaswa kuwepo na mamlaka kwenye kanisa? Toa mifano.

Biblia inarejea kuwepo kwa mamlaka kwenye kanisa katika maeneo mengi. [1] (Baadhi ya mifano ni Waebrania 13:7, 17; Tito 1:5; Warumi 12:8; 1 Wakorintho 14:40; na 1 Timotheo 5:17.)

Kufafanua uongozi kama ushawishi kunatusaidia sisi kuona majukumu ya uongozi katika kanisa. Baadhi ya majukumu maalumu yamewekwa na Mungu ili kwamba viongozi waweze kupatikana na kupewa nguvu za kuongoza kanisa katika kukamilisha malengo yake.

► Mwanafunzi anapaswa asome Waefeso 4:11-12 kwa ajili ya kikundi.

[2]Siyo majukumu yote maalumu yanayoweza kutambuliwa pamoja na miito maalumu katika orodha hii. Kwa mfano. Mwanamuziki au kiongozi wa ibada siyo mojawapo katika hivi. Hata hivyo, kila jukumu la uongozi wa huduma unapaswa uelekeze fokasi yake katika kulisaidia kanisa kukamilisha malengo yake.

Majukumu ya uongozi hayako tu katika kuhubiri, kufundisha, na uinjilisti. Jukumu la kanisa ni pana kuliko mambo haya. Watu wa kanisa pia hufanya kazi katika kufikia mahitaji ya vitendo. Mtu anayeongoza watu kuchangia vifaa kwa ajili ya kutengeneza bustani analisaidia kanisa katika kukamilisha malengo yake. Majukumu ya kanisa huleta ulazima wa majukumu mengi ya uongozi kuliko yale yanayotokea ndani ya jengo la kanisa.


[1]Kama mtu yeyote katika kikundi atabishana kwamba uongozi katika kanisa siyo muhimu na siyo kibiblia, kikundi kinaweza kuyapima maandiko yaliyoandikwa ndani ya alama za kufunga na kufungua. Jaribu kuepuka kutumia muda mrefu katika jambo hili.
.
[2]

“Nilikuwa namwomba Mungu aweze kunisaidia. Kisha nikamwomba kama mimi ninaweza kumsaidia yeye. Niliishia katika kumwomba afanye kazi yake kupitia kwangu.”

- J. Hudson Taylor