Utangulizi
Ujenzi wa hekalu umeanza. Ni msingi tu ambao umeshajengwa, lakini hayo yalikuwa ni mafanikio makubwa. Umati wa watu ulikusanyika kusherehekea. Watu wengi walikuwa wakipiga kelele kwa shangwe na kumtukuza Mungu. Lakini wakati wazee walipouona ule msingi, walitambua kwamba hekalu jipya halitakuwa zuri kabisa kuliko lile la mwanzo. Walilia kwa masikitiko kwamba lile hekalu kubwa walilokuwa wanalikumbuka lilikuwa limeondoka kabisa. Masikitiko na shangwe vilikuwa vimechangamana kutoa katika zile sauti za umati wa watu. Ilikuwa ni wakati wa mabadiliko makubwa, na watu walikuwa na hisia tofauti kuhusu vipengele tofauti kwa ajili ya mabadiliko (Ezra 3:10-13).