Malengo ya Somo
(1) Mwanafunzi ataweza kueleza:
-
Jinsi tunavyojua kwamba mfano wa Mungu katika ubinadamu si mfano wa kimwili.
-
Sifa nane za mfano wa Mungu katika ubinadamu.
-
Kwamba watu wameumbwa kimahususi kwa ajili ya kuwa katika uhusiano na Mungu.
-
Maana ya jinsi watu wana uhuru wa kuchagua.
-
Kwamba watu wana thamani isiyo na kipimo zaidi ya thamani yao ya kiutendaji katika maisha ya kidunia.
-
Kauli ya kanuni za Kikristo kuhusu ubinadamu.
(2) Mwanafunzi ataelewa kwamba hawezi kuridhika akiwa mtu asiye na uhusiano na Mungu.