Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 9: Uwasilishaji wa injili “Daraja”

6 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

Kumbukumbu kwa Kiongozi wa Darasa: Mwanzoni mwa kipidi hiki, wanafunzi watapaswa kutoa taarifa ya uzoefu wao wa ushirikishaji wa Injili kwa kutumia mbinu iliyoko kwenye somo lililopita. Kumbuka kwamba wanafunzi wanahitaji kutiana moyo mmoja kwa mwingine. Kila mwanafunzi aliyeshirikisha injili amekamilisha jambo fulani la muhimu sana hata kama msikilizaji wake hakuonyesha uwajibikaji ulio chanya.

Kwenye maandalizi ya somo hili, hakikisha kwamba una ubao wa kuandikia kwa chaki, ubao mweupe au makaratasi makubwa kwa ajili ya kuelezea michoro kwa wanafunzi wa darasa.

Hilo tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo (1 Yohana 1:3).

► Je, kuna sababu gani aliyoitoa mtume kuhusiana na kushirikisha injili?

Tumepata uzoefu wa nini maana ya kukutana na Mungu na kuokoka, kwa ajili ya kuanzisha uhusiano pamoja naye. Pia tuna uhusiano na watu wengine ambao nao wako kwenye uhusiano na Mungu. Tunaposhirikisha injili, tunawakaribisha watu wengine kuja kwenye uhusiano ambao na sisi tunao pamoja na Mungu na wngine wanaomjua yeye.