Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 7: Maombi na Kufunga

10 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

Kile ambacho kanisa linahitaji kwa wakati wa sasa siyo mashine zaidi au kitu kingine cha ziada, siyo mashirika mapya au ziada ya hayo, na siyo mbinu mpya, bali wanahitajika watu ambao Roho Mtakatifu anaweza akawatumia—watu wa maombi, watu wenye uwezo mkubwa kwenye maombi. Roho Mtakatifu hatiririki kupitia mbinu zilizopo, bali kupitia watu. Roho Mtakatifu haji juu ya mashine, bali juu ya watu. Roho Mtakatifu haachilii upako wake kwenye mipango, bali kwa watu—watu wa maombi.[1]

► Je, kuna kosa gani ambalo E. M. Bounds anajaribu kulisahihisha kupitia taarifa zilizoko hapo juu?

Kitendo cha maombi hutoa taarifa ya utegemezi kwa Mungu, Mtu ambaye anashughuli nyingi kwenye mambo yake hata akashindwa kuomba anafikiri kwamba kazi yake ni muhimu zaidi kuliko kazi ambayo Mungu ataifanya katika kujibu maombi yake.

Kwa kuwa sisi ni tegemezi kwa Roho Mtakatifu, maombi ni muhimu sana kwetu. Paulo aliwataka watu waombe kwa ajili ya kuieneza injili (2 Wathesalonike 3:1, Wakolosai 4:3, Waefeso 6:19).


[1]E. M. Bounds, Power through Prayer, Accessed from https://ccel.org/ccel/bounds/power/power.I_1.html on January 13, 2023