Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 15: Mpango wa Kanisa

10 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

Eric anapenda kuzungumzia kuhusu miaka ya awali ya kanisa lake. “Tulianza kwa kukutanika kwenye bustani ya kupumzikia, tukimkaribisha kila mtu tuliyemwona. Wakati wa kipindi cha baridi, tulikutanikia kwenye basi mbovu la zamani. Hatukuwa na vyumba vya maliwato. Baadaye, tulihamia katika ukumbi wa michezo ya mazoezi ya viungo kwa muda, kisha tukapangisha nafasi kwenye jengo moja la zamani la kanisa.”

Kanisa la Eric lilikuwa linakua katika miaka hiyo. Watu waliokuwa wamejitoa kwa ajili ya kanisa hawakuwa wamevutiwa na jengo la kanisa. Walikuwa wamevutiwa na kundi la watu.

Kwenye somo hili, tunapozungumzia kuhusu mpango wa kanisa, hatuzungumzii kuhusu jengo la kanisa. Makanisa mengi makubwa wanayo maelezo kuhusiana na jinsi walivyoanza wakiwa katika mazingira magumu.

Baadhi ya makanisa yanasema kwamba hayawezi kuwa kivutio kwa watu kwa sababu majengo yao hayaridhishi kwa uzuri. Ukweli ni kwamba wanakosa kitu kingine ambacho ni muhimu sana kuliko hata jengo.