Utangulizi
[1]► Soma Mathayo 18:2-6, 10-14. Je, kuna maonyo gani tunayoyaona katika aya hizi? Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuelezea umuhimu anaouna Mungu kwa watoto?
Mara nyingine watu husema kwamba watoto ni muhimu kwa sababu ni kizazi cha kesho, ni kanisa la baadaye, na viongozi wa baadaye. Hayo yote ni kweli; lakini mwanzo wa yote, watoto ni muhimu kwa sababu wao ni watu. Mara nyingine wazazi huonekana kusahau kwamba watoto ni watu wenye roho za milele na umaarufu na wana nguvu ambazo hazijaonekana bado.
Mtu mmoja msafiri alisimama kwenye kijiji kimoja kidogo. Alimwona babu mmoja akiwa amekaa kando ya barabara na akasema, “Sijawahi kamwe kusikia lolote kuhusu kijiji hiki kabla ya hapo. Je, watu maarufu hawakuwahi kuzaliwa hapa? Yule babu akajibu, “Hapana. Ni watoto tu.”