Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 2: Theolojia ya Kuzaliwa mara ya Pili

13 min read

by Stephen Gibson


Ukumbusho kwa kiongozi wa darasa

Pamoja na nyongeza ya aya za Maandiko zitakazojadiliwa katika somo hili, Kuna aya nyingine nyingi zilizoonyeshwa kwenye tanbihi. Inawezekana kusiwepo na muda wa kutosha kwa darasa kupitia na kuzisoma aya zote wakati wa kipindi cha darasani. Kiongozi wa darasa anaweza kuchagua baadhi kwa ajili ya kusomwa.

Neno kuokoka linahusika na mabadiliko yanayotokea wakati mtu anapookoka. Kusudi la uinjilisti ni kumwongoza mwenye dhambi aweze kufikia kuokoka.

► Soma 1 Wathesalonike 1. Je, kuna mabadiliko gani ya ndani kwa Wathesalonike wakati walipookoka

Ili kuelewa ni kwa nini mtu anahitajika kuokoka, na kuelewa ni nini kinachotokea wakati mtu anapookoka, ni lazima tuelewe hali ya mtenda dhambi kabla ya kuokoka.