Ukumbusho kwa kiongozi wa darasa
Pamoja na nyongeza ya aya za Maandiko zitakazojadiliwa katika somo hili, Kuna aya nyingine nyingi zilizoonyeshwa kwenye tanbihi. Inawezekana kusiwepo na muda wa kutosha kwa darasa kupitia na kuzisoma aya zote wakati wa kipindi cha darasani. Kiongozi wa darasa anaweza kuchagua baadhi kwa ajili ya kusomwa.
Neno kuokoka linahusika na mabadiliko yanayotokea wakati mtu anapookoka. Kusudi la uinjilisti ni kumwongoza mwenye dhambi aweze kufikia kuokoka.
► Soma 1 Wathesalonike 1. Je, kuna mabadiliko gani ya ndani kwa Wathesalonike wakati walipookoka
Ili kuelewa ni kwa nini mtu anahitajika kuokoka, na kuelewa ni nini kinachotokea wakati mtu anapookoka, ni lazima tuelewe hali ya mtenda dhambi kabla ya kuokoka.