► Mwanafunzi atapaswa kusoma 1 Wakorintho 1:17-25 kwa ajili ya kikundi. Je, mbinu ya Mungu ya kuokoa watu waliopotea ni ipi?
Wayahudi walikuwa wanatafuta nguvu za kulikomboa taifa lao. Walihitaji ujumbe wa nguvu pamoja na alama za nguvu kuthibitisha kwamba itafanya kazi.
Mataifa walikuwa wanatafuta hekima ya kuelewa maisha na kwa ajili ya kupata mafanikio katika dunia. Walihitaji ujumbe ambao ungewafafanulia jinsi ya kupata kile walichokuwa wanahitaji.
Msalaba uliwakilisha kujisalimisha na dhabihu. Kwa Wayahudi ambao walikuwa wanataka nguvu, ilionekana kama ni udhaifu. Kwa Mataifa ambao walitaka hekima ya kidunia, ilionekana kama ni upumbavu. Kiuhalisia, nguvu na hekima ya Mungu ilidhihirishwa katika kifo cha Kristo. Msalaba ulionekana kama ni udhaifu na upumbavu wa Mungu, lakini ulikuwa ni bora zaidi kuliko juhudi nyingi sana za wanadamu.
Ujumbe wa injili uko kinyume na vitu, na tamaa za dhambi za kibinadamu. Unatoa wito wa kutubu na kujisalimisha kwa Mungu. Unaonekana kama ni ujumbe wa kipumbavu, kwa sababu watu wanataka kusikia kuhusu jinsi ya kupata kile wanachokitaka.
Mungu amechagua kutumia injili kwa ajili ya kuokoa watu. Ametoa jukumu la mawasiliano kwa waamini. Neno kuhubiri halina maana ya kurejelea kwa mtu anayezungumza na umati wa watu tu, bali ni kwa mawasiliano ya injili kwa njia mbalimbali. Kiini cha kifungu siyo kwamba kuhubiri hadharani ndiyo mbinu ya Mungu iliyochaguliwa. Kiini ni kwamba injili ni mbinu ya Mungu.
► Je, kifungu kinamaanisha nini kinaposema kwamba kuhubiri kuhusu msalaba ni upumbavu kwa wale wasioamini?
Neno kuhubiri linaweza kutumika katika ufahamu mpana zaidi katika kurejelea kwenye aina mbalimbali za kuwasilisha Neno la Mungu. Hata hivyo, kwenye somo hili, tutatumia neno kuhubiri katika hali yake ya kawaida: ikirejelea kwa mtu kuzungumza Neno la Mungu kwenye kongamano la watu.
Kuhubiri Kiuinjilisti ni wakati ambapo injili inawasilishwa kwenye kongamano la watu. Siyo tu hali ya kuwasilisha kichwa cha habari chochote au kifungu cha Maandiko. Ni uwasilishaji wa injili.
Mhubiri wa kiinjili kwa kawaida hushawishi wasikilizaji wake kuchukua hatua za mara moja kutokana na ujumbe, kwa lengo kwamba watabadilika mara moja. Ujumbe umeandaliwa kwa ajili ya kuwaleta kwenye huo uamuzi.
Taarifa iliyoko kwenye ujumbe wa kiinjili unachambuliwa kwa umakini sana. Kusudi la ujumbe kimsingi siyo kwa ajili ya elimu, Mhubiri hujaribu kutoa taarifa ambayo wasikilizaji wanaihitaji kwa ajili ya kufanya maamuzi na kubadilika. Taarifa hii huhusisha pamoja na ufafanuzi wa injili ya msingi, jinsi msikilizaji atakavyokuwa na mwitikio, na uwezekano wa madhara ya uamuzi.
Mahubiri yanaweza yakafanyika kwenye eneo lenye ukimya, lililopangika vizuri kama vile kusanyiko la wafuasi wa kanisa kwenye jengo la kanisa au kwenye eneo lingine lenye umati mkubwa wa watu waliokusanyika kwa ajili ya malengo mengine. Inawezekana kusanyiko likawa rafiki na ujumbe wa injili, au wanaweza wasikubali.
► Je, ni maeneo gani tofauti yaliyoandaliwa ambayo umewahi kuona injili ikihubiriwa?
Miongozo kuhusiana na Kuhubiri Kiuinjilisti
Kwa kuwa kuna tofauti kati ya kuhubiri ndani ya kanisa na kuhubiri kwenye kikundi kingine kilicho tofauti, kwanza tutatoa miongozo ambayo inatumika kwenye mahubiri ya kiuinjilsti katika kanisa. Kwenye sehemu nyingine huko mbele ya somo hili, tutatoa baadhi ya miongozo ambayo inatumika kwenye mahubiri ya nje.
(1) Elezea kwa kinaganaga kifungu cha andiko.
Neno la Mungu lina nguvu sana, kwa hiyo mhubiri anahitajika kulitumia. Siyo lazima kwamba kifungu kiwe kirefu sana au mhubiri atumie muda mrefu akielezea kwa undani kilichopo. Anapaswa atumie Maandiko yanayounga mkono ujumbe wa injili. Anapaswa ahakikishe kwamba kauli zake nyingi anazozitoa zina msingi wa Maandiko, ili nguvu ya Neno la Mungu iweze kutumika. Hapaswi kuchagua sehemu ya aya kwa ajili ya kutumia kwenye maana nyingine tofauti na ile maana iliyoko kwenye maudhui yake.
(2) Unapaswa afafanue maana za maneno toba na imani.
Wasikilizaji wanaweza wakawa na mawazo potofu kuhusiana na maana za maneno haya. Wanaweza wakafikiri kwamba toba maana yake ni kufanya maisha yako yawe mazuri zaidi ili uweze kukubalika na Mungu. Wanahitaji kujua kwamba toba maana yake ni kuwa na majuto ya kutosha kutokana na dhambi zako kiasi kwamba uko tayari uondolewe kutoka katika hizo dhambi.
Wasikilizaji wanaweza kufikiri kwamba imani maana yake ni kuamini katika dini au kutekeleza mila na taratibu za dini. Wanahitaji kujua kwamba imani inayookoa inakufanya uweke utiifu wako kabisa kwenye kifo na mateso ya Kristo msalabani kwa ajili ya wokovu.
(3) Sisitiza kwamba mtu huwa ni Mkristo mara tu anapookoka.
Watu wengi wana mawazo potofu kuhusu nini maana ya kuwa Mkristo na ni kwa jinsi gani mtu anaweza akawa Mkristo. Wanaweza wakadhania kwamba mhubiri anawataka tu wazidi kuwa watu wa dini au wawe sehemu ya kanisa. Wanaweza wakafikiri kwamba anawataka tu waanze kuishi maisha ya utiisho mkali. Sisitiza kwamba wakati wa mabadiliko mwenye dhambi hutubu, akapokea msamaha, na kuanza uhusiano wake binafsi na Mungu.
(4) Kataa au pinga sababu za kupotosha walizo nazo watu kwa kukiri kuwa ni Wakristo.
Kwnye jamii kadhaa, watu wengi wanafikiri kwamba wao ni Wakristo. Wanaweza wakafikiri kwamba wao ni Wakristo kwa sababu wamekuweko makanisani, wamefanya matendo mema, wanaamini baadhi ya mambo, au wamekuwa na uzoefu kidogo wa kiroho. Mbali na kusisitiza mabadiliko, elezea maisha yenye uhusiano na Mungu na utii unaotakiwa ambao unafuata baada ya kufanya toba.
(5) Hakikisha kwamba watu wasiokuwa wa makanisa wanakuelewa.
Usitumie maneno ambayo watu wa kidini tu ndio wanaoyafahamu. Usirejelee kwenye mila na taratibu za kidini ambazo hawawezi kuzielewa.
► Je, ni baadhi ya maneno gani yanayotumika katika kanisa lako ambayo watu katika ujirani wako wanaweza wasielewe?
(6) Toa msamaha, uhusiano na Mungu, na uzima wa milele.
Hizi ndizo faida muhimu zaidi za kuokolewa. Onyesha uzito wa hali ya mtenda-dhambi kwa kueleza hukumu na adhabu ya milele itakayowapata watenda-dhambi.
(7) Epuka kutoa ahadi za mafanikio ambazo hazijawahi kuahidiwa kwenye injili.
Kama watu wanafikiri kwamba kuokoka kunahusisha pamoja na kupata faida ya mali kutoka kwa Mungu au kanisa, mafanikio, kuponywa magonjwa, au aina nyingine yeyote ya kuendeleza hali ya maisha, watakuwa wamejaribu kupata hizo faida bila ya kutubu kwa uhakika.
Unaweza ukaelezea kwamba wakati Mungu akiwa katika uthibiti wa maisha ya mwanadamu, ataongoza, atabariki, na atakuwa ni msaada kwenye matatizo yao. Hata hivyo, hatupaswi kutoa ahadi kwamba matatizo yao yote yatatatuliwa kama watakuwa Wakristo. Kwa baadhi ya watu wengine, maisha yanaweza kuwa magumu zaidi kwa sababu ya mateso.
(8) Usiunganishe kuokoka kwa mtu na uanachama wa kanisa la mahali pamoja.
Uanachama wa kanisa utapatikana mara tu baada ya mtu kubadilika kwa ukweli, lakini vigezo vya uanachama vinahitajika vielezwe baada ya mabadiliko. Usizungumzie kuhusu mahitaji ya kuwa mwanachama wakati unapojaribu kumshawishi mtu aweze kutubu dhambi zake. Mwinjilisti atapaswa kujielekeza katika kumleta msikilizaji kwenye kukutana na Mungu.
► Je, kuna baadhi ya mahitaji gani ya uanachama katika kanisa lako ambayo siyo muhimu kwa ajili ya kuokoka?
(9) Usiweke viwango kwa ajili ya mabadiliko yanayoendana na kukua.
Mwite msikilizaji ajitokeze kwa ajili ya kutubu dhambi zake anazozifahamu. Usimweleze masharti kuhusiana na undani wa maisha ambayo hatawza kuelewa hadi hapo atakapokuwa amekuwa Mkristo kamili kwa muda fulani. Wito wa toba na imani una matatizo ya kutosha. Usiongeze matatizo yatakayoweza kumfanya mtu aikatae injili.
(10) Fafanua unataka watu wafanye nini.
Usitake kudhania kwamba msikilizaji anajua kwamba anapaswa kuomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msamaha. Usitake kudhania kwamba anajua jinsi ya kujitokeza mbele na kupiga magoti. Wakati unapowaalika wasikilizaji ili wajitokeze, wafafanulie kabisa ni kitu gani unataka wafanye. Tafakari ni kwa jinsi gani utafanya mambo yawe mepesi kwa kadri itakavyowezekana kwa mtu ambaye ni mwepesi kutishwa na mazingira ya kanisa.
Kuomba na wenye Mahitaji
Watu wanaweza wakakusanyika kuomba madhabahuni kwa sababu nyingi. Mara nyingine mchungaji anaweza akawaalika watu kwa ajili kuombea mahitaji mbalimbali. Miongozo iliyoorodheshwa hapa haimaanishi kwamba ni lazima itumike kwenye nyakati zote za maombi ya madhabahuni. Miongozi hii inatumika katika kuomba pamoja na wale ambao wameitikia wito wa mwaliko baada ya mahubiri ya kiuinjilisti.
Mchungaji anapaswa ahakikishe kwamba baadhi ya watu wa kanisa wamefundishika katika kuwasaidia watu wanaoomba kwa ajili ya kuokoka. Atapaswa kuwa na watu hawa wakiwa wamejiandaa kusaidia wakati atakapotoa wito wa mwaliko wa kiuinjilisti.
Mara nyingine mtu anayetaka kusaidia kuomba na watu wengine anakuwa ni kikwazo badala ya msaada. Mchungaji atapaswa kuyaangalia matatizo akiwa madhabahuni na kuwa tayari kutoa msaada. Kama mtu anakuwa kikwazo kwenye muda wa maombi madhabahuni kwa tabia isiyokuwa ya hekima au ushauri mbaya, mchungaji atafanya kila linalowezekana kusahihisha tatizo hilo.
Tunaamini kwamba mtu anaweza kutubu, akaamini, na kujionea mabadiliko mara moja. Imani hiyo inaongoza busara ya kuomba na wenye mahitaji.
Miongozo ya kuomba na Waombaji waliona hitaji
(1) Angalau mwamini mmoja aliyekomaa atapaswa kumsaidia kila mwenye hitaji la maombi.
Usimwache mwenye mahitaji ya maombi aombe peke yake na kuondoka madhabahuni bila ya msaada. Tunataka mwenye mahitaji ya maombi afikie ushindi kamili.
(2) Tafuta ni kwa nini mwenye mahitaji anaomba.
Usitake kudhania kwamba anaomba kwa ajili ya kuokoka. Hata baada ya mahubiri ya kiuinjilisti kumalizika, watu huja kwenye madhabahu kwa sababu nyingi. Siyo lazima kumsumbua mwenye mahitaji ya maombi akiwa katika maombi; lakini wakati mwingine, mwamini anayemsaidia anaweza akamwuliza, “Je, unataka Mungu akufanyie nini?” Kisha mwamini anaweza akaomba pamoja naye kwa hitaji lolote alilo nalo.
(3) Mtie moyo mwenye mahitaji ya maombi afanye toba kamili.
Uliza, “Je, uko tayari kutubu dhambi zako, na umruhusu Mungu akukomboe kutoka katika dhambi yako?” Mtie moyo amwambie Mungu kuhusu toba yake. Siyo lazima kwake kukiri dhambi zake kwa mchungaji au mtu mwingine yeyote, labda iwe kuna dhambi maalumu dhidi ya watu hao.
(4) Mhakikishie mwenye mahitaji ya maombi kwamba Mungu atamsemehe.
Mwambie amwombe Mungu kwa ajili ya msamaha na atii ahadi ya Mungu ya kusamehe. Kama itaonekana anapata shida kutokana na kuwa na mashaka, mwoyeshe ahadi ya kimaandiko (1 Yohana 1:9, Yohana 3:16, Warumi 5:8).
Kama itaonekana mwenye mahitaji ya maombi anashindwa kuomba kwa maneno yake mwenyewe, msaidizi anaweza akamsaidia maombi ambayo itampasa arudie ayafuatishe. Inaweza ikawa kama maombi yafuatayo:
“Bwana, ninajua mimi ni mwenye dhambi na ninayestahili adhabu ya milele. Ninajutia dhambi zangu na niko tayari kuachana nazo. Ninaomba unisamehe, siyo kwa sababu ninastahili, bali kwa sababu Yesu alikufa kwa ajili yangu. Asante kwa wokovu wako. Kuanzia sasa, nitaishi kwa ajili yako tu.”
Kwa kawaida, kama mwenye mahitaji ana ugumu wa kuomba na kupata ushindi kamili, itakuwa kuna dhambi ambayo hajawa tayari kuachana nayo. Hawezi kuwa na imani kwa ajili ya msamaha hadi pale atakapokuwa ametubu kwa ukweli.
(5) Mtake mtu aliyeokoka akupe ushuhuda.
Kama mwenye mahitaji ya kuomba ataonekana anapata ushindi, mtu atapaswa kumwuliza, “Je, Mungu alikufanyia nini?” Mtie moyo atoe kauli yenye msimamo. Anaweza akatoa ushuhuda kwenye mkusanyiko wa waumini, lakini atapaswa angalau kwa mtu ambaye alisaidiana naye katika kuomba.
(6) Toa maelezo yaliyochapishwa kuhusiana na wokovu.
Mtu aliyebadilika anapaswa apewe maelezo yaliyochapishwa kuhusiana na wokovu ili aondoke nayo. Yanapaswa yawe yanaelezea kuhusu wokovu. Yatamsaidia mtu huyu kuelewa ni nini kilichotokea na pia yatamsaidia katika kuelezea kwa watu wengine.
(7) Andaa hatua ya kwanza ya kufanya huduma ya ufuasi.
Hatua ya kwanza ya kufanya huduma ya ufuasi kwa kawaida itakuwa ni kukutana na mchungaji au mwamini aliyekomaa kiroho. Hakikisha mtu aliyebadilika anaelewa ni nini kilichotendeka kwake. Baada ya hapo, anaweza kujiunga na kikundi kidogo au kuwa anakutana na mwamini mwingine mara kwa mara.
Inatakiwa kuwe na mtu wa kutembelea familia yake, kuhakikisha wanajua kuhusu mabadiliko yao, na kuwakaribisha kuhudhuria kwenye kanisa. Inawezekana kukawepo na nafasi ya kushirikishana injili pamoja nao.
► Je, kuna mila na taratibu gani katika kanisa lako kwa ajili ya kuomba na mtu mwenye mahitaji ya maombi? Unahitaji ufanye nini ili kuongezea orodha iliyotajwa hapo juu?
Kuhubiri kwenye Mkutano wa Nje
Kuhubiri kwenye mkutano wa nje ni kwa kusudi la kuwafikia watu ambao hawaji kanisani. Ni vigumu sana kwa sababu wasikilizaji wako pale kwa makusudi mengine na wanaweza wasiwe makini na kinachoendelea. Inawezekana kukawepo na makelele na mambo ya uvurugaji. Kunakuwa hakuna mazingira ya kuabudu yaliyoandaliwa na kusanyiko la kanisa kama ambavyo ingewezekana ikawa ndani ya kanisa.
Hitaji la wazi la kwa mhubiri wa mkutano wa nje ni kwamba anatakiwa awe na sauti yenye nguvu ya kutosha kwa ajili ya watu kumsikia, au anaweza kutumia vyombo vya kupaazia sauti.
Changamoto ya kwanza ya kuhubiri kwenye mkutana wa nje ni kupata utulivu na usikivu wa makini. Watu walioko kwenye eneo la mkutano huamua mara moja kama wanataka kusikiliza au la. Baadhi yao watasikiliza kwa dakika chache. Wengi wao watasikiliza sentensi mbili au tatu kabla hawajaamua kama wanayo au hawana nia ya kuendelea kusikiliza.
Mhubiri anapaswa atumie sentensi fupi, na kila sentensi iwe na maudhui ya kutosha. Ni lazima akumbuke kwamba kila sentensi ni lazima iwe sentensi ya kwanza ambayo baadhi ya wasikilizaji wataisikia. Kuwa na pointi ya kusemea kwenye kila sentensi kutasaidia kugusa usikivu wa makini wa wasikilizaji. Kama atafanikiwa kupata kundi la kumsikiliza, anaweza kutoa vielelezo na kufafanua pointi zake kwa ufasaha zaidi.
Ikiwezekana, mhubiri atapaswa kuwa na kikundi cha waamini pamoja naye. Kama watu wanaopita wakiona kuna watu wengine wanaosikiliza, na wao pia kuna uwezekano mkubwa wakasimama na kusikiliza. Kama kuna wana muziki wa maudhui ya Kikristo ambao wanaweza kuwa wanatumbuiza nyimbo kabla ya kuhubiri, kwa kawaida husaidia katika kuwakusanya watu.
Mhubiri anapaswa awakaribishe watu wasogee kule mbele aliko yeye na kuwaombea kwa ajili ya wokovu.
Wasaidizi watapaswa kugawa vipeperushi vyenye taarifa zilizochapishwa kwa watu katika eneo hilo.
► Je, kuna utaratibu gani uliopo kwa ajili ya mahubiri ya mkutano wa nje katika maeneo ya majirani zako?
Ukumbusho kwa Kongozi wa Darasa
Sasa kila mwanafunzi aangalie mahubiri yake ya kiuinjilisti aliyokuja nayo. Ayafanyie tafakuri ni kwa jinsi gani yanatimiza miongozi 10 ya mahubiri ya kiuinjilisti. Atapaswa kupanga ni kwa jinsi gani yatakavyoweza kufanyiwa mapitio ili kusahihisha na kufanya yawe bora zaidi.
Inawezekana kusiwe na muda wa kutosha wa kujadili mahubiri ya kila mwanafunzi aliyoandaa, lakini baadhi yao miongoni wao watapaswa watoe mahubiri yao yajadiliwe ili kuonyesha mifano.
Katika kipindi kitakachofuata cha darasa hakutakuwepo na somo lingine. Wanafunzi watapaswa washughulike na kuwasilisha mahubiri ya kiuinjilisti waliyoyaandaa na kisha kuyajadili. Siyo lazima wafanye mahubiri yote hadi kukamilisha kabisa, lakini yafupishwe na yawekwe kwenye muhtasari ambao kila mahubiri yanaweza kuwasilishwa kwa takribani dakika 5-7. Kipindi kingine cha darasa kitakachofuata baada ya kipindi cha mazoezi kitakuwa kwenye somo la 12.
Kazi ya Kufanya
Tayarisha mahubiri ya kiuinjilisti ambayo yatazingatia mtiririko wa miongozo iliyotolewa katika somo hili. Hayo mahubiri siyo lazima yaandikwe yote kwa ukamilifu, lakini yatapaswa yawe na taarifa za msingi zilizoandikwa. Ziletwe kwenye kikao cha darasa kitakachofuata kwa ajili ya majadiliano.
SGC exists to equip rising Christian leaders around the world by providing free, high-quality theological resources. We gladly grant permission for you to print and distribute our courses under these simple guidelines:
No Changes – Course content must not be altered in any way.
No Profit Sales – Printed copies may not be sold for profit.
Free Use for Ministry – Churches, schools, and other training ministries may freely print and distribute copies—even if they charge tuition.
No Unauthorized Translations – Please contact us before translating any course into another language.
All materials remain the copyrighted property of Shepherds Global Classroom. We simply ask that you honor the integrity of the content and mission.