Utangulizi
Somo linalohusu zaka ni lenye kuelekea kuleta mabishano kwenye maeneo mengine. Watu wengine wanafikiri kwamba wazo la utoaji wa zaka halikubaliani au halipatani na wokovu kwa njia ya imani. Wanasema inaelekea kana kwamba ni malipo kwa ajili ya wokovu. Watu wengine hawataki kujisikia wana jukumu la kutoa msaada kwa kanisa. Wanatoa tu kile wanachojisikia kutoa ili mradi ametoa. Katika somo hili tutaangalia kwenye misingi ya Biblia na makusudi ya vitendo ya zaka.
► Je, ni mambo gani umesikia kutoka kwa watu wakisema sababu zilizo kinyume na utoaji wa zaka?