Mwanzo wa Desturi ya Ubatizaji
► Mwanafunzi atapaswa kusoma Mathayo 3:1-12 kwa ajili ya kikundi.
Kwenye Agano Jipya, tunatambulishwa dhana ya ubatizo kupitia huduma ya Yohana Mbatizaji. Hata hivyo, Yohana hakuanzisha ubatizo. Mafarisayo waliwabatiza Mataifa walioamini na kuingia katika Uyahudi. Mafarisayo Hawakuwabatiza Wayahudi, kwa sababu walichukulia kwamba Wayahudi tayari walikuwa ni watu wa Mungu. Yohana alitekeleza kwa jinsi ya tofauti kabisa desturi hii kwa sababu yeye aliwabatiza Wayahudi.
► Je, Yohana alimkataa nani kwenye ubatizo? Kwa nini? Hali hiyo inatufahamisha nini kuhusiana na hitaji la ubatizo?
Baadhi ya Mafarisayo walijitokeza ili wabatizwe na Yohana, lakini Yohana aliwakataza kwa sababu walikuwa hawajatubu.
Mafarisayo walidhania kwamba wao hawakuwa na hitaji la kutubu na kupata msamaha kwa sababu walikuwa Wayahudi. Yohana aliwataka waelewe kwamba watu halisi wa Mungu ni wale wanaompenda na kumtumikia yeye. Watu wanaojinadi kuwa wao ni watu wa Mungu kwa sababu ya kuzaliwa kama Wayahudi ni kama miti ya matunda ambayo haizalishi matunda. Mungu aliwakataza.
► Mwanafunzi atapaswa kusoma Yohana 3:22-23 na Yohana 4:1-2 kwa ajili ya kikundi.
Ni dhahiri kwamba Yesu alisisitiza kuhusu ubatizo katika huduma yake. Yesu mwenyewe hakubatiza, lakini aliikabidhi jukumu hilo kwa wanafunzi wake. Walibatiza watu wengi kuliko hata ilivyokuwa kwa Yohana.
► Mwanafunzi atapaswa kusoma Mathayo 28:18-20 kwa ajili ya kikundi.
Mwishoni mwa huduma ya Yesu hapa duniani aliwaagiza wanafunzi wake waende mahali popote duniani wakawafanye watu kuwa wanafunzi. Aliwaagiza wabatize.
Tunajua kwamba agizo hili halikuwa tu kwa ajili ya mitume, kwa sababu huduma ya umisheni itachukua karne nyingi kumalizika. Yesu alitoa ahadi kwamba atakuwa pamoja nao “hadi mwisho,” hii ikionyesha kwamba hili agizo na ahadi hii ni kwa ajili ya kanisa katika vizazi vyote.
Tunaona kutoka katika nyaraka za Agano Jipya kwamba kanisa la karne ya kwanza lilitii agizo hili neno kwa neno (Matendo 2:38, Matendo 8:38).
► Mwanafunzi atapaswa kusoma 1 Wakorintho 1:12-17 kwa ajili ya kikundi. Kwa nini Paulo alifurahia kwamba yeye mwenyewe hakubatiza watu wengi katika Korintho?
Ubatizo uliwakilisha kuingia kwenye kanisa. Kanisa la Korintho lilikuwa limegawanyika na waumini wake wanachama walikuwa wanafuata viongozi mbalimbali. Paulo anawakumbusha kwamba ubatizo hauna maana kwamba watu wanafanyika kuwa ni wafuasi wa mtu fulani; bali inamaanisha kwamba wanafanyika kuwa ni wafuasi wa Kristo. Alikuwa amefurahia kwamba yeye mwenyewe hakuwa amebatiza watu wengi miongoni mwao, ili kwamba hakuna mtu yeyote atakayefikiria kwamba alikuwa anawataka wawe wafuasi wake binafsi. Kipaumbele cha Paulo kilikuwa ni kuhubiri injili.
► Kifungu hiki kinatuambia nini kuhusiana na zoezi la kawaida la ubatizo kwenye kanisa la mwanzo?
Kifungu hiki kinatuambia kwamba kanisa la mwanzo lilibatiza waumini kila mahali. Walikuwa wanafuata agizo la Yesu. Ubatizo haukuwa tu kwa ajili ya watu katika Israeli. Haikuwa ni desturi ya muda mfupi tu. Ilifanyika kila mahali ambapo injili ilikwenda.
[1]Tangu mwanzo, kanisa limekuwa likifanya huduma ya ubatizo kama ushuhuda katika jamii au kwa jamii hadharani kwamba mwenye dhambi ametubu na ameingia kwenye ushirika wa watu walioamini.
Kwa watu wengi, ubatizo siyo katika wakati ambapo wanafanyika kuwa Wakristo. Mwenye dhambi anayetubu anakuwa ameokoka na wakati huo yeye mwenyewe akiwa ameiweka imani yake kwa Kristo. Baada ya kuwa ameokoka, anapaswa aheshimu na kutii agizo la kubatizwa kama udhihirisho wa maisha yake mapya ya utiifu kwa Yesu kama Bwana na Mwokozi. Kuna watu ambao ni tofauti, kwa sababu ilikuwa wakati wa ubatizo ni kwamba waliiweka imani yao katika Kristo na uzoefu wa kuokoka. Lakini, kwa kawaida, ubatizo ni ushuhuda kwamba wokovu tayari umeshatokea.
► Je, utamwambia nini mtu anayesema kwamba alifanyika Mkristo wakati alipobatizwa?
“Ubatizo wa Kikristo ni sakramenti inayoandamana na ibada za kidini kuashiria kukubalika kwa faida zinazotokana na kufa na kufufuka kwa Yesu Kristo, na ahadi iliyo na kusudio kamili la utiifu katika utakatifu na haki.”
- Wiley & Culbertson,
Introduction to Christian Theology