Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa
Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 12: Nidhamu ya Kanisa

15 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

Katika Somo la 3, tulijifunza tafsiri hii kuhusiana na kanisa la Mahali au mtaa:

Kanisa la mahali ni kikundi cha waumini ambacho kinafanya kazi kama familia ya kiroho na jamii ya imani; wakitoa injili na ushirika wa kanisa kwa kila mtu anayetubu; wakitekeleza tendo la ubatizo na ushirika wa meza ya Bwana, wakishirikiana katika kumwabudu Mungu, ushirika, uinjilisti, uanafunzi, na kukamilisha kazi ya mwili wa Kristo kwa karama za Roho Mtakatifu; waliojitoa kabisa kwa ajili ya Neno la Mungu; wakiwa na umoja ulio katika msingi wa mafundisho ya imani ya kibiblia, wakiwa na uzoefu wa neema, na maisha ya Roho Mtakatifu.

Sasa tutafakari tafsiri ya nidhamu ya kanisa.

Tafsiri ya Nidhamu ya kanisa

nidhamu ya kanisa ni umoja wa kanisa, wenye lengo la kuwajibisha dhambi inayotendwa na mwanachama kukiwa na makusudi manne ya kulinda um/oja wa kanisa, kusimamia ukweli, kulilinda kusanyiko kutokana na ushawishi mbaya, na kumrejesha tena mwanachama aliyeanguka dhambini kwenye wokovu na ushirika.

► Angalia tafsiri ya kanisa na tafsiri ya nidhamu ya kanisa. Kwa kuzingatia kanisa ni nini, elezea ni kwa nini nidhamu ya kanisa ni muhimu.