Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa
Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 2: Umoja wa Kikristo

14 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

► Itampasa mwanafunzi asome hadithi ifuatayo ya kufikirika kwa ajili ya darasa.

Wakati mmoja kulikuwepo na jiji ambalo lilikuwa hatarini kukumbwa na mafuriko ya mto. Watu wa jiji hilo walijipanga katika vikundi mbalimbali vya kujaza mifuko ya mchanga na kuiweka kwenye kingo za mto huo. Watu walifanya kazi kwa shauku kubwa, na hamasa ya kila kikundi iliongezeka. Baadaye vile kikundi vilijipa majina. Kulikuwa na kikundi cha waokoaji wa jiji, Wasawazishaji Mchanga, na Wathibiti Mto. Utambulisho wa kikundi ulikuwa jambo muhimu sana. Wanachama wa kila kikundi walivaa fulana zinazofanana. Walizungumzia ni kwa jinsi gani kikundi kimoja kilikuwa ni bora kuliko kikundi kingine. Kila kikundi kililaumu kazi ya kikundi kingine.

Wakati kikundi cha wathibiti Mto kilipokwenda kuomba toroli kutoka kwenye kikundi cha Waokoaji wa Jiji, hawakuwaruhusu kulichukua toroli hilo, kwa sababu walidhania kwamba wanaweza wakalihitaji tena baadaye. Wakati kikundi cha Wasawazishaji Mchanga walipopungukiwa na mifuko ya kuwekea mchanga, ilibidi wasubiri kwa takribani saa moja kwa ajili ya mifuko kuletwa, ingawaje vikundi vingine vilikuwa na mifuko ya ziada. Vikundi vyote vilikuwa vimejisahau kwamba wote kwa pamoja walikuwa na jukumu moja. Mafanikio ya kila kikundi yalionekana ni muhimu zaidi kuliko matokeo ya ujumla ya jukumu lote lililokuwepo.

► Ni kwa jinsi gani makanisa yanafanya kama ilivyokuwa kwa vikundi vilivyoko kwenye hadithi hii?

Biblia inasisitiza kwa kina sana kuhusu thamani ya umoja wa Kikristo. Paulo alikemea utengano au mafarakano ya kanisa la Korintho kwa kuuliza swali, “Je! Kristo amegawanyika?” (1 Wakorintho 1:13). Aliwaambia Waefeso kudumisha umoja wa Roho. Akionyesha kwamba, “Mwili mmoja... Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja” (Waefeso 4:4-5). Yesu aliomba kwa bidii sana ili kwamba waumini kuwa kitu kimoja, ili ulimwengu upate kuamini kwamba Yesu alitoka kwa Baba (Yohana 17:21).

Tangu mwanzo, kanisa lilijifikiria lenyewe kuwa ni moja. Imani ya Mitume inahusisha pamoja na taarifa hii: "Naamini… kanisa takatifu la Kikristo (katholiko) lililo moja tu; ushirika wa watakatifu.” Imani ya Nikea inahusisha pamoja na taarifa hii: "Twaamini Kanisa moja (katholiko) la Kikristo la ulimwengu wote na la kimitume.” Neno katholiko lina maana ya kamilifu na ulimwengu wote. Neno kimitume linamaanisha kwamba kanisa lilianzishwa na mitume na hata sasa linafuata mafundisho ya mitume.

Matamko ya imani ya awali yalionyesha imani muhimu za mafundisho ya Kikristo. Kanisa halikuhusika na mtu yeyote ambaye hakukubaliana na matamko haya ya imani, kwa kuwa yalikuwa yamekusudiwa kutoa ufafanuzi wa mambo muhimu ya Ukristo. Kwa hiyo, mtu alionekana kuwa ni mwenye ukengeufu kama alikuwa anafikiria kwamba kuna makanisa ya kweli ambayo siyo sehemu ya kanisa moja la ulimwengu wote.

Madhehebu

Kanisa duniani halijawahi kuundwa likawa shirika moja kwa karne nyingi. Badala yake, kuna makundi mengi ya makanisa yanayotofautiana. Kundi moja la makanisa linalounda shirika moja linaitwa dhehebu.

Katika mwaka 451 B.K. Othodoksi ya Mashariki lilijiengua kutoka katika Ukatoliki wa Kirumi kwa sababu ya kutokubaliana katika mafundisho ya imani. Leo hii kuna mashirika mengi ya makanisa katika Othodoksi ya Mashariki: Koptiki, Othodoksi ya Ethiopia. Othodoksi ya Eritrea, Malankara ya Syria, Syriaki, na dhehebu la kitume la Armenia.

Katika mwaka 1054 B.K. Othodoksi ya Mashariki lilijiengua kutoka katika Ukatoliki wa Kirumi. Leo hii kuna mashirika kumi na tano ya makanisa katika Othodoksi ya Mashariki ikiwa ni pamoja na Kanisa la Kiothodoksi la Urusi, Kanisa la Kiothodoksi la Serbia, na Kanisa la Kiothodoksi la Syprusi.

Mbali na mgawanyiko huu mkubwa, makundi mengine ya makanisa katika karne zile yalijiengua kutoka katika kanisa Katoliki.

Matengenezo ya Kanisa la Kiprotestanti yalitokea mnamo miaka ya 1500. Makanisa mengi yalijiengua kutoka katika Ukatoliki wa Kirumi kwa sababu waliamini kwamba Kanisa Katoliki halihubiri tena wazi wazi injili ya kweli. Kulikuwa na mambo mengine mengi, yakiwemo mambo ya kisiasa, lakini mafundisho ya imani ndiyo yaliyokuwa muhimu zaidi.

Madhehebu mengi yaliundwa kutoka katika Matengenezo. Kanisa la Uingereza liliundwa na makanisa mengi yaliyokuwepo katika nchi ya Uingereza. Ilipotokea kuanzishwa kwa makanisa yao katika nchi nyingine nje ya Uingereza, yalijulikana kama Kanisa la Kiangilikana.

Makanisa ya Wapresibiteri yalitokana na ushawishi wa wana Matengenezo: Yohana Calvin nchini Switzerland, Yohana Knox nchini Scotland, na wengineo. Siku hizi kuna madhehebu mengi ya Wapresibiteri.

Kanisa la Kilutheri lilianzishwa nchini Ujerumani kutokana na huduma ya Martin Luther. Kuna makanisa mengi ya Kilutheri kwa sasa katika nchi mbalimbali duniani.

Wafuasi wa Anabaptisti waliamini kwamba matengenezo hayakukamilisha urejeshwaji wa injili ya kimaandiko. Waliamini kwamba kuabudu hakupaswi kuwa ni sherehe zisizokuwa za kimaandiko na kwamba ubatizo ulipaswa uwe tu ni kwa ajili ya watu waliookoka na siyo kwa watoto wadogo. Kutokana na wao, kumejitokeza madhehebu mengi ya Kibaptisti katika nchi mbalimbali duniani.

Makanisa ya Kipentekoste yalianza kutokana na Uamsho mkubwa uliofanyika Los Angeles Marekani mnamo mwaka wa 1906. Mchanganyiko mkubwa wa madhehebu ya Kipentekoste na Karismatiki yapo katika maeneo mengi ya dunia. Madhehebu haya yana mchanganyiko wa aina nyingi za mafundisho ya imani.

Yako madhehebu mengi kwa maelfu ambayo yanajinadi kwamba wao ni Wakristo. Yako makanisa mengi yaliyo huru ambayo siyo sehemu ya madhehebu.

Mara nyingi madhehebu yanaanza na kikundi cha watu ambao wanaamini kwamba ukweli fulani umekataliwa au umepuuzwa na kanisa wanaloshiriki. Wanaanza na dhehebu dogo kwa nia ya kutaka kuwa sahihi katika mafundisho ya imani. Wakati mwingi wanaendelea kutengeneza mafundisho yao ya imani, na wanakuwa tofauti na madhehebu mengine. Pia wanatengeneza mila tofauti kuhusu namna sahihi ya ibada na mambo ya kina yanayohusiana na jinsi ya kuishi Kikristo.

Wakati mwingine madhehebu huanza kwa kufanywa huduma ya uinjilisti. Kama kutatokea kuwepo na watu wengi waliookoka katika eneo hilo na hakuna dhehebu litakaloweza kuendelea kuwatunza, dhehebu jipya linaweza kuanzishwa. Dhehebu linaweza kuanza kutokana na kazi ya shirika la umisheni katika nchi maalumu husika.

Madhehebu mengi ya Kikristo hayajinadi kama ndiyo pekee Wakristo wa kweli. Kama shirika litajinadi kwamba ndilo kanisa lote la Mungu katika ulimwengu, halipaswi kuwa la kuaminika.

► Je, kuna aina ngapi tofauti za majina ya makanisa na madhehebu unazozifahamu?

Watu wasioamini wanapingana na Ukristo kwa sababu ya mgawanyiko wake mwingi uliopo na aina nyingi zilizopo. Watu wengi wasioamini wanafikiri kwamba aina mbalimbali za vikundi vyote vya Kikristo vinajichanganya kimoja kwa kingine. Watu wengi wa dunia wanafikiri kwamba hakuna aina ya umoja unaoeleweka miongoni mwa Wakristo.

► Je, kuna tabia gani ambazo zinaonekana kama zinakataa umoja miongoni mwa makanisa?

Makanisa yanaonekana kuwekea mkazo mambo ambayo yanafanya yaonekane kuwa tofauti na makanisa mengine, hata kama mambo hayo siyo mafundisho ya msingi ya imani. Wakati mwingine makanisa huharakisha kulaumu makanisa mengine kwa ajili ya unafiki na kukubaliana katika mambo yasiyotakiwa kukubaliana, au dhambi nyinginezo, bila ya kuelewa kwa uhakika. Baadhi ya makanisa husema kwamba makanisa mengine siyo ya Kikristo, ingawaje yanaamini kwenye msingi wa mafundisho ya imani ya Ukristo.

Makanisa hayaonekani kuwa yenye umoja katika kuendelea Agizo Kuu la Yesu. Makanisa yanaonekana kushindana kama yanayofanya biashara. Viongozi wengi hudhania kwamba ni kupoteza nguvu na mapato yao kama watajihusisha katika kusaidia huduma ambazo hazina majina ya mashirika yao.

Labda Wakristo wote watakubaliana kwamba Wakristo wote wanapaswa wawe na umoja, lakini wanaweza wasijue ni aina gani ya umoja unaotakiwa. Kwanza, tutazungumzia kuhusu umoja wa kanisa la duniani kote; kisha, tutazungumzia kuhusu umoja wa Kanisa la mahali/mtaa.

Umoja wa Kanisa la Duniani Kote: Siyo Muungano wa Mashirika

Baadhi ya watu wanafikiri kwamba makanisa yote yanapaswa yaungane yawe shirika moja. Wanafikiri kwamba uwepo wa mashirika mengi yaliyojitenga yenyewe inamaanisha kwamba kanisa haliko katika umoja. Hawatofautishi kati ya kiini au kitovu cha kanisa na mashirika ya kanisa; kwa hiyo, kwao inamaanisha umoja ni kuungana kwa mashirika.

► Je, utasema nini kwa mtu anayefikiria kwamba Mashirika na Makanisa yote ye Kikrsto yanapaswa yaungane yawe shirika moja?

Mashirika hayawezi yakaunganika bila ya kuamua kwamba tofauti zao za mafundisho ya imani siyo kitu cha kuzingatia. Kuwa na umoja ni lazima kuwepo na kukubaliana kwenye baadhi ya mafundisho ya misingi ya imani, na iamuliwe kwamba wingi wa mafundisho yao mengine ya imani hayana umuhimu sana wa kutosha kuwatenganisha kutokana na wale wasiokubaliana nao.

Jaribio lote zima la kutaka kuunganisha makanisa yote yawe katika shirika moja yako kwenye msingi kwamba umoja wa Kikristo ni umoja unahusiana na Mashirika. Yesu mwenyewe hakuwahi kudai kwamba wafuasi wake wote wawe kwenye shirika moja linalofanana wakati wa huduma yake hapa duniani, kama inavyoonekana katika tukio hili hapa chini:

Yohana akajibu akamwambia; Bwana mkubwa, tuliona mtu anatoa pepo kwa jina lako; tukamkataza, kwa sababu hafuatani na sisi. Yesu akamwambia, Msimkataze, kwa kuwa yeye ambaye si kinyume chenu yu upande wenu (Luka 9:49-50).

Maneno haya ya Yesu yanaonyesha kwamba mtu anaweza akawa “hafuatani na sisi” (siyo sehemu ya shirika letu), lakini bado akawa “yu upande wetu.” Ni wazi kwamba, kuna umoja wa Kikristo ambao hauoneshi kwamba kuna uwepo wa kuwa katika shirika moja.

Kwa karne nyingi tangu wakati wa huduma ya Yesu hapa duniani kumekuwepo na mashirika mengi yaliyojinadi kwamba ni kanisa la dunia nzima, wakisema kwamba hakuna mashirika mengine yasiyokuwa pamoja nao yanayopaswa kudai kwamba wao ni Wakristo. Yesu hakuwahi kudai kwamba kundi lake la wanafunzi ndilo kanisa lote hata wakati ambapo alikuwa pamoja nao kimwili akiwaongoza.

Wakati mwingine watu hutumia neno kanisa lisiloonekana. Neno kanisa lisiloonekana linarejelea kwenye ukweli kwamba hakuna shirika linaloonekana kuwa na orodha ya wanachama yenye kujumuisha wakristo wote. Pia, mashirika ya Kikristo yana wanachama ambao siyo Wakristo wa kweli. Kwa hiyo, hatuwezi kuelekeza kwa shirika lolote maalumu na kusema kwamba hili ndilo kanisa la ulimwengu wote.

Ingawaje kanisa la dunia siyo shirika moja, umoja miongoni mwa Wakristo wote unapaswa uwe unaonekana. Yesu aliomba kwamba waumini wawe na umoja na akasema kwamba matokeo yatakuwa kwamba dunia itamwamini yeye (Yohana 17:21). Hii inamaanisha kwamba umoja wa Kikristo unapaswa kwa namna fulani uwe unaonekana kwa Wakristo na ulimwengu wote.

► Je wakati unapokutana na mtu anayejinadi kwamba mimi ni Mkristo, ni mambo gani muhimu kwako unayoweza kushirikishana naye kuhusiana na umoja wa Kikristo?

Msingi wa Umoja wa Kikristo

Umoja wa Kanisa la mahali uko kwenye msingi wa mafundisho ya imani ya Biblia, uzoefu wa neema, na maisha ya Roho Mtakatifu. Umoja wa Wakristo mbali na Kanisa la mahali una msingi unaofanana, ingawaje undani wake ni mdogo.

Njia nyingine ya kuweza kuelezea msingi wa umoja ni hii: Kama mtu atashuhudia kwamba ameokoka, ikaonekana ana maisha ya kiroho, na ikaonekana anaamini katika misingi ya Ukristo wa kweli, basi ushirika wa Kikristo unawezekana. Ushirika unaweza ukaendelea kwa muda wote ali mradi mtu anaonekana kuishi kwenye ushirika na Mungu na katika kuitii Biblia.

Umoja wa Kikristo hautegemei kuwepo na kukubaliana na kila kipengele cha mafundisho ya imani. Siyo jambo rahisi kwa Kanisa katika maeneo yote kukubaliana mambo yote kwa undani yanayohusiana na mafundisho ya imani. Hata mitume walikuwa na mambo ambayo hawakukubaliana (Wagalatia 2:11-14).

Makundi ya waumini hujifunza Biblia na kujadiliana katika yale wanayoamini, wakijaribu kuhakikisha kwamba yako sahihi. Wanatambua kwamba hawakubaliani na mafundisho ya imani ya baadhi ya makundi mengine ya Wakristo.

[1]Yapo baadhi ya mafundisho ya imani ambayo ni ya msingi na ya muhimu kwa imani ya Mkristo. Kama mtu hataamini haya mafundisho ya imani, hawezi akaelewa na kuiamini injili.

Kisha kuna orodha ndefu ya mafundisho ya imani ambayo kanisa fulani huamini. Makanisa mengi yanaelewa kwamba, siyo Wakristo wote katika maeneo yote wanaokubaliana na mafundisho yote ya imani. Hata kama fundisho la imani liko katika Biblia, siyo kila mtu atakayeweza kuielewa Biblia kwa njia inayofanana.

► Je, mifano ya msingi ya mafundisho ya imani ni ipi? Kuna mifano gani mingine ambayo siyo ya msingi?

Baadhi ya misingi ya imani ni kuhusiana na asili ya Mungu, Uungu wa Yesu na Roho Mtakatifu, Kufa na kufufuka kwa Kristo, na wokovu ni kwa neema kwa njia ya imani.

Baadhi ya mafundisho ya imani ambayo siyo ya msingi ni imani kuhusiana na aina za kuabudu na undani wa maisha ya Kikristo. Ni muhimu kwetu kuwa watu wa kibiblia zaidi katika kufanya mambo yote, lakini tunapaswa tutambue kwamba siyo Wakristo wote wa kweli watakaoweza kukubaliana na undani wa mambo haya yote.


[1]

" Kama moyo wako uko sahihi, kama moyo wangu na wako ulivyo, basi nipende kwa upendo wa moyo wako, kama rafiki wa karibu kuliko kaka mtu; kama kaka katika Kristo, raia mwenzako wa Yerusalemu mpya, askari mwenzako anayepigana vita vinavyofanana, chini ya akida yule yule wa wokovu wetu. Nipende kama mshiriki mwenzako katika ufalme na subira ya Yesu, na mrithi wa pamoja wa utukufu wake.”

- John Wesley,
"Roho ya Umoja” (“The Spirit of Unity")

Ishara za Kanisa la Kweli

Mtazamo wa ishara za kanisa la kweli ulishikiliwa kwa pamoja na Kanisa Katoliki na wanamatengenezo. Kwa karne nyingi Wakristo walikuwa wakiamini kwamba ishara nne za kanisa la kweli ni umoja, utakatifu, ukatoliki, na utume. Maneno haya manne yamekuwa yakitafsiriwa kwa njia tofauti.

Hapa kuna tafsiri chache rahisi. Umoja inamaanisha kwamba kanisa linahusisha Wakristo wote wa kweli, ingawaje siyo lazima wawe kwenye orodha rasmi. Utakatifu inamaanisha kwamba kanisa linasimama kinyume na dhambi na linaamini kwamba wokovu ni kuachana na mambo ya dhambi. Ukatoliki inamaanisha kwamba linaweza kuchukua muundo unaofaa kwenye utamaduni yeyote mahali popote, wakati likiendelea kushikilia kwenye ukweli muhimu. Utume inamaanisha kwamba kanisa linashikilia kwenye imani yake ya asili iliyoanzishwa na mitume.

Kosa la Kanisa Kushindana

Wakati mwingine makanisa katika maeneo yanakuwa karibu karibu sana kiasi kwamba watu wanaweza wakachagua ni kanisa gani la kwenda. Watu katika kanisa moja wanaweza kujaribu kuonyesha kwa jamii kwamba kanisa lao ni bora zaidi kuliko makanisa mengine yote. Wanashindana na makanisa mengine, wakijaribu kulifanya kanisa lao liwe la kuvutia zaidi kuliko makanisa mengine. Wanafikiri kwamba kanisa lao lina mafanikio zaidi kama idadi ya watu itakuwa inaongezeka.

Mashindano baina ya makanisa yako kwenye msingi wa kukosa uelewa wa kanisa. Watu wengi wanaelekea kufikiri kwamba kanisa ni kama biashara ambayo inapaswa iwe kivutio kwa watu wengine au wateja wake. Au, ni kama eneo la maonyesho ambalo linapaswa liweze kuwa kivutio kwa hadhira. Haya yote ni mitazamo potofu kuhusiana na kanisa.

Kanisa ni familia ya kiroho. Wanachama wa familia nzuri kila mmoja hujaribu kuchukua jukumu la kumjali mwenzake. Wanafanya kazi pamoja kwa ajili ya kupata vigezo vya familia. Wanatumia muda wao wakiwa pamoja kwa sababu ya uhusiano wao.

Kanisa ni familia ya watu wenye imani, yenye msingi wake kwenye uhusiano na Mungu pamoja na wao wenyewe. Wanahitaji wanachama wapya ambao watakuwa wamevutiwa na injili na maisha ya kiroho ya familia hiyo. Kanisa linapaswa liwe na mwelekeo wa kushirikisha injili na kudhihirisha uhai wa kanisa. Kisha watawavutia watu walio sahihi, watu ambao wako tayari kuwa sehemu ya familia hiyo.

► Je, kama kanisa linajaribu kushindana na makanisa mengine yaliyoko kwenye eneo moja, ni kwa jinsi gani mashindano hayo yataweza kulibadilisha kanisa?

Umoja wa Kanisa la mahali.

► Je, ni kwa nini Kanisa la mahali linahitaji makubaliano ya mafundisho mengi zaidi ya imani kuliko umoja wa Kikristo wa dunia?

Mkristo anaweza akakubaliana na ushuhuda wa Wakristo wengine ambao hawashikamani na mafundisho yake yote ya imani, ali mradi yawe yanashikamana na msingi wa mafundisho ya imani ya Kikristo na yanadhihirisha maisha ya Kikristo. Hata hivyo, kwa kuwa Mkristo ni lazima yeye binafsi ayafanyie kazi yale anayoamini kwamba ni sahihi, hawezi akajiunga katika huduma ya Wakristo wa aina zote. Kwa mfano, kama mchungaji anaamini kwamba Biblia inamwambia abatize watu waliookoka, hawezi akawa mchungaji wa watu ambao wanafundisha kwamba watu wanaookoka hawatakiwi kubatizwa.

Mfano mwingine: Kama mtu anaamini kwamba karama ya kunena kwa lugha siyo ushuhuda wa mtu kuwa amejazwa na nguvu za Roho Mtakatifu, itakuwa ni vigumu kwake kushikamana na huduma ya watu ambao wanaamini kwamba mtu ambaye hazungumzi kwa lugha hana nguvu za Roho Mtakatifu. Kutakuwepo na matatizo katika ushirika wao kwa sababu hawatakubaliana na ushuhuda wake. Kutakuwepo na matatizo katika ushirikiano kihuduma kwa sababu watakuwa wanajaribu kuwaongoza watu wapya waliookoka kwenye uzoefu wa kuzungumza kwa lugha.

Kama mtu atakuwa anafanya mambo ambayo anajua kwamba kibiblia ni makosa, atakuwa anakiuka dhamira yake mwenyewe. Anakuwa amejiweka mwenyewe chini ya hukumu ya Mungu kwa sababu amechagua kufanya jambo fulani ambalo anaamini kabisa kwamba Biblia imelikataza (tazama Warumi 14:22-23).

Mkristo anaweza akaamini kwamba watu wanaoamini mafundisho ya imani mbali mbali, ndiyo Wakristo wa kweli na sahihi, lakini ni lazima awe kwenye ushirika na kufanya huduma kwenye kundi la watu wanaokubaliana na mafundisho mengi zaidi ya imani. Hii inamaanisha kwamba Kanisa la mahali ni lazima liwe na tamko la fundisho la imani litakalokuwa zaidi ya mafundisho ya msingi ya kanisa la ulimwengu wote.

► Je, kwa nini inakuwa ni makosa kwa mtu kujaribu kuamini kila mafundisho ya imani ya makanisa?

Hitimisho

Mkristo ni lazima aweke uwiano wa tabia yake dhidi ya watu wengine. Hawezi akasema kwamba Wakristo wengine siyo Wakristo wa kweli kwa sababu ya kutofautiana kwenye mafundisho ya imani madogo madogo ambayo siyo yale ya msingi. Hata hivyo, Mkristo ni lazima awe na ushirika wa karibu na Kanisa la mahali ambalo linasimamia mafundisho ya imani kwa pamoja ambayo yanawawezesha kufanya ushirika na huduma pamoja.

Taarifa Saba kwa Muhtasari

1. Biblia imeweka mkazo kuhusu Umoja wa Kikristo.

2. Kanisa la kwanza liliamini katika umoja wa kanisa kama fundisho la imani la msingi.

3. Kanisa haliwezi kukamilisha umoja kwa kuwaweka Wakristo wa mashirika yote katika shirika moja.

4. Umoja wa Kikristo una msingi wake kutoka katika fundisho la Biblia, uzoefu wa neema, na maisha ya Roho Mtakatifu.

5. Wakristo mahali popote wanakubaliana kwenye baadhi ya mafundisho ya imani ya msingi ya Ukristo.

6. Wakristo katika makanisa mbalimbali hawatakubaliana juu ya maelezo ya kina ya mafundisho ya imani.

7. Kanisa la mahali ni lazima likubaliane na maelezo ya kina ya mafundisho mbalimbali ya imani.

Kazi za Kufanya Somo la 2

1. Kariri taarifa Saba kwa Muhtasari kwa ajili ya somo la 2. Andika aya moja inayoelezea maana na umuhimu wa kila kipengele katika hizi Taarifa Saba kwa Muhtasari (jumla aya saba) kwa mtu ambaye siyo wa darasa lako. Wakilisha kwa kiongozi wako wa darasa kabla ya kuanza kwa kipindi cha darasa kinachofuata. Kuwa tayari kushirikisha aya moja kwa kikundi kama kiongozi wa darasa atakutaka ufanye hivyo wakati wa majadiliano. Andika Taarifa hizi kutoka kwenye ufahamu wako bila ya kuangalia mahali popote mwanzoni mwa kipindi cha darasa kinachofuata.

2. Wakati wa hii kozi, utahitajika kufundisha somo, au sehemu ya somo, kwa mtu binafsi au kikundi ambacho siyo sehemu ya darasa lako. Unaweza kuchagua maudhui ya kufundisha. Itakupasa ufanye hivyo mara tatu, kwa kutumia mafundisho tofauti. Fanya mpangilio wako mwenyewe wa nafasi za kufundisha na toa taarifa kwa kiongozi wa darasa baada ya kuwa umemaliza kufundisha.

3. Masailiano: Ongea na washirika wa makanisa matatu tofauti na uwaulize ni kwa jinsi gani wanavyoyaona makanisa mengine. Je, ni umoja gani wanaofikiria kwamba utafaa kuwepo miongoni mwa Wakristo wote? Andika ibara moja inayohusiana na mazungumzo uliyoyafanya na kila mmoja wa watu hawa watatu.

Next Lesson