Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa
Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 13: Tabia ya Kiongozi wa Kikristo

12 min read

by Stephen Gibson


Changamoto ya Uongozi wa Kikristo

Andiko tunalokwenda kujifunza katika somo hili linahusika mahususi kwa wachungaji na mashemasi, lakini pia kwa viongozi wengine katika kanisa. Mtu yeyote anayefundisha darasa, anayeongoza katika nyumba ya kanisa, au anayeongoza ibada pia ni kiongozi. Watu hao wote ni mfano wa aina ya watu wa kuigwa waliothibitishwa na kanisa. Kwa hiyo, ni muhimu kwamba wawe ni mfano mzuri wa tabia ya Kikristo.

Tabia binafsi ya kiongozi ni muhimu zaidi kuliko hata uwezo wake wa asili alio nao. Mungu humpa kiongozi wa Kikristo uwezo unaohitajika kwa ajili ya huduma.

► Mwanafunzi atapaswa kusoma 1 Timotheo 3:1-7 kwa ajili ya kikundi.

Siyo vibaya kwa mtu kuwa na matamanio ya nafasi ya uchungaji kama anakuwa anayo nia sahihi. Kama atakuwa ni mtu anayetaka apewe heshima na mamlaka au nafasi ya kujipatia faida ya fedha, mtu kama huyu hana moyo wa kichungaji. Anapaswa atamani nafasi ya kuhudumu.

Tuna aya mbili za maandiko kuhusu sifa za wachungaji na mashemasi. Ziliandikwa na mtume Paulo kwa Timotheo na Tito. Timotheo alikuwa kiongozi wa makanisa yaliyokuwepo Efeso; Tito alikuwa kiongozi wa makanisa ya Krete. Walikuwa na kazi ya kuteua wachungaji kwa ajili ya kila kanisa la mtaa.

Jaribu kufikiria ilikuwaje kwa mtu kuwa mchungaji katika karne ya kwanza ya kanisa! Alikuwa hajawahi kuwa na mafunzo ya kitaaluma. Hakukuwa na vitabu kuhusiana na huduma kwa ajili yake ili ajifunze. Hakuwahi kuwa na nafasi ya kuangalia wanavyofanya wachungaji wengine. Hakuwahi kuwa hata na nafasi ya kuangalia maisha ya kanisa kwa muda mrefu kwa sababu kanisa lilikuwa jipya. Hata sehemu kubwa ya Agano Jipya ilikuwa bado kuandikwa.

Paulo alimwambia Timotheo jinsi ya kupata heshima kutoka kwa watu wake. Alimtaka awe kielelezo katika usemi, na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi (1 Timotheo 4:12). Mchungaji hapewi heshima kwa kudai aheshimiwe.

► Je, ni kwa jinsi gani mchungaji hupata heshima?

Mtume aliwaeleza Timotheo na Tito sifa zinazohitajika kwa ajili ya kuwa mchungaji. Sifa nyingi zimerejea kwenye tabia na kukomaa Kikristo kuliko vipaji au uwezo binafsi wa mtu. Kwa hiyo, kila Mkristo anapaswa kutiwa moyo kusitawisha sifa hizo.