Utangulizi
► Je, mtu anaweza akawa Mkristo na akaishi maisha ya Ukristo bila ya kuwa na kanisa?
[1]Kuna sababu nyingi ambazo watu wanaweza wakawa nazo kwa ajili ya kuja kanisani. Mtu anaweza kuja kanisani kwa ajili ya kujifunza, kuuhisi uwepo wa Mungu, kupata kibali cha kukubalika na urafiki, kutiwa moyo, kubadilishwa, kumwabudu Mungu pamoja na washirika wengine, kudhihirisha kujikabidhi kabisa kwa Mungu na watu wake, kusaidia katika huduma za kanisa, na kutaka kuona kwamba ni kitu gani Mungu atatenda.
Kama mtu atakuwa haingii kwenye kanisa, mambo yaliyoorodheshwa hapa juu hayana umuhimu kwake. Atakuwa ni mtu wa aina gani asiyejali mambo hayo? Kuwepo katika kanisa siyo uthibitisho kwamba mtu ni Mkristo, lakini kama mtu hahudhurii katika kanisa, inawezekana akawa siyo Mkristo
► Je, kwa nini uanachama wa kanisa ni jambo la kujali sana? Je, haitoshi tu mtu kwenda kanisani na akafanyika kuwa Mkristo?
“Wale watu wa mwanzo walioamini walilipenda kanisa kwa sababu walimpenda Yesu.”
- Larry Smith, I Believe: Fundamentals of the Christian Faith