Kanisa baada ya Pentekoste
► Mwanafunzi atapaswa kusoma Matendo 2:42-47 kwa ajili ya darasa. Ni maelezo gani unayoyaona kuhusiana na ushirika wa kanisa baada ya Pentekoste?
Mara tu baada ya Pentekoste, kitabu cha Matendo kinaelezea kuhusu maisha ya kanisa. “Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika.” Watu wengi waliuza vitu vyao ili kusaidia maisha ya jamii ya kanisa. Walikuwa wakikutana mara kwa mara katika hekalu kwa ajili ya ushirika wa kumsifu Mungu na pia wakikutana kwa ajili ya ushirika wa nyumba kwa nyumba.
[1]Kwenye kipindi ambacho utendaji wa Roho Mtakatifu ulikuwa wa hali ya juu miongoni mwao, maisha ya jamii ya kanisa nayo yalikuwa katika kiwango cha juu sana. Kwa wale waumini wa mwanzo, kuwa sehemu ya kanisa ilimaanisha ni zaidi ya kushiriki kwenye ibada za Jumapili. Kila siku waumini walishirikishana kwa pamoja kuhusu maisha yao.
“Kwa pamoja kwenye Maandiko na kanuni za imani ushirika wa Kikristo unawakilishwa kama namna ya neema.”
- Wiley & Culbertson,
Introduction to Christian Theology