Utangulizi
► Je, kanisa la mahali ni kitu gani? Je, lina tofauti gani na aina nyingine zote za vikundi?
Tafsiri hii ya kanisa la mahali inaweza kugawanywa kwenye maeneo makuu saba muhimu. Maeneo haya yanaelezewa kwa uwazi zaidi katika kozi hii yote.
Ufafanuzi ya Kanisa la mahali Kanisa la mahali ni kikundi cha waumini ambacho kinafanya kazi kama familia ya kiroho na jamii ya imani; wakitoa injili na ushirika wa kanisa kwa kila mtu anayetubu; wakitekeleza tendo la ubatizo na ushirika wa meza ya Bwana, wakishirikiana katika kumwabudu Mungu, ushirika, uinjilisti, uanafunzi, na kukamilisha kazi ya mwili wa Kristo kwa karama za Roho Mtakatifu; waliojitoa kabisa kwa ajili ya Neno la Mungu; wakiwa na umoja ulio katika msingi wa mafundisho ya imani ya kibiblia, wakiwa na uzoefu wa neema, na maisha ya Roho Mtakatifu. |
[1]Hapa chini sehemu za tafsiri hiyo zimerejewa zikiwa na maelezo yaliyofuatana nazo.
► Kwa kila kipengele kinachofuata, jadili ni kwa nini ni muhimu kuwepo na tabia hii ya kanisa. Je, ni matokeo gani yatakayoonekana kama kanisa litakosa kuwa na tabia hii?
Kanisa la mahali ni kikundi cha waumini ambacho kinafanya kazi kama familia ya kiroho na jamii ya imani…
Kanisa ni kikundi kilichoanzishwa kutokana na imani ya Kikristo. Kina mahusiano mazito kuliko hata kikundi kingine katika dunia.
[2]…wakitoa injili na ushirika wa kanisa kwa kila mtu anayetubu…
Kanisa haliwezi kuwatenga watu wa kikundi cha utamaduni fulani au kabila fulani au kwa madaraja ya watu na bado likandelea kuwa mwaminifu kwa injili. Hakuna umuhimu wa mambo ya utamaduni au kabila, au madaraja ya kijamii. Pia, kanisa haliwezi kukataa kusamehe baadhi ya dhambi kama limesimama kwenye uaminifu wa injili.
…wakitekeleza tendo la ubatizo na ushirika wa meza ya Bwana…
Yesu alitoa maagizo kwa kanisa kwa ajili ya kutekeleza sherehe hizi. Ubatizo unawakilisha kuingia katika kanisa kwa kuokoka. Ushirika wa meza ya Bwana unamaanisha neema inayodhihirishwa kutoka katika injili.
…wakishirikiana katika kumwabudu Mungu, ushirika, uinjilisti, na uanafunzi…
Haya ni makusudi ya msingi ya kanisa. Ushirikiano ni muhimu kwa ajili ya kanisa kukamilisha makusudi muhimu.
…kukamilisha kazi ya mwili wa Kristo kwa karama za Roho Mtakatifu…
Majukumu ya kiroho ya kanisa kamwe hayawezi kukamilishwa kwa uwezo wa kibinadamu peke yake.
…waliojitoa kabisa kwa ajili ya Neno la Mungu…
Kanisa linaitegemea Biblia kwa ajili ya injili yake, mafundisho ya imani, na mamlaka. Kama kanisa litachagua kutokuitii Biblia, kanisa litakuwa limepoteza mamlaka yake kwa ajili ya kufundisha.
…wakiwa na umoja ulio katika msingi wa mafundisho ya imani ya kibiblia, wakiwa na uzoefu wa neema, na maisha ya Roho Mtakatifu.
Washirika wa kanisa wanaweza wakajikabidhi mmoja kwa ajili ya mwingine kwa sababu wanayo haya mambo matatu kwa pamoja. Bila ya haya mambo matatu, ushirika wa kweli wa Kikristo hautawezekana kuwepo.
“Watu walioamini hawajaitwa kibinafsi kuishi tu kwa kuwa na uhusiano binafsi na Mungu bali wameitwa kwa pamoja na kushikamanishwa kwa pamoja kama watu.”
- Thomas Oden,
Life in the Spirit
“Kanisa la Kristo linaloonekana ni mkusanyiko wa watu waaminifu ambao Neno kamilifu la Mungu linahubiriwa na sakramenti zinatolewa kwa mujibu wa agizo la Kristo…”
- Kanuni za Dini
za Kanisa la Methodisti