Malengo ya Somo
Hadi kufikia mwishoni mwa somo hili, mwanafunzi atapaswa:
(1) Kuelezea sifa na tabia za upendo wa kweli.
(2) Kufafanua inamaanisha nini kumpenda mtu bila masharti.
(3) Kuelezea umuhimu wa kuthibitisha upendo kwa lugha ya msingi ya upendo ya mtu.
(4) Kutumia maneno ya kuthibitisha katika kuonyesha upendo na uthamini kwa ajili ya sifa binafsi za mwanafamilia, sifa bainishi za tabia na sifa bainishi za nafsi ya mtu.