Malengo ya Somo
Hadi kufikia mwishoni mwa somo hili, mwanafunzi atapaswa:
(1) Kuelewa jinsi ndoa inavyotakiwa kuakisi mahusiano yaliyoko katika Utatu Mtakatifu wa Mungu.
(2) Akubaliane na mpango wa Mungu kuhusu kupata watoto.
(3) Kuelewa jinsi Anguko la mwanadamu lilivyoathiri ndoa na mahusiano ya kifamilia.
(4) Athamini jinsi mapenzi ya Mungu yanavyokuwa yanatekelezwa licha ya kasoro za kibinadamu zilizopo.
(5) Atambue kwamba utiifu kwenye mpango wa Mungu unaweza ukaisaidia familia yeyote kuwa familia ya ukombozi.