Njia Tatu za Kutumia Sura hii
-
Mwezeshaji anaweza kutumia njia zilizomo katika sura hii ili kuendeleza walimu wenyeji. Kama kanisa mahali lilipo halina mtu anayejisikia ana uwezo wa kufundisha, mwezeshaji hawezi kuanza haraka masomo yanayojitegemea. Mwezeshaji lazima amgundue na kumwedeleza mwalimu mtarajiwa. Sura hii inamwelezea mwezeshaji jinsi ya kupata mwalimu mwenyeji.
-
Mwezeshaji kutayarisha walimu wenyeji jinsi ya kutumia mbinu hii kwa wanafunzi wao. Kama walimu wenyeji wa eneo jipya tayari wana uwezo wa kufundisha, mwezeshaji hahitaji kutumia zoezi katika sura hii. Mwezeshaji anapaswa kujifunza mbinu hii kwa walimu wenyeji ili waweze kutumia mazoezi ya kuwaendeleza washiriki.
-
Mwalimu mwenyeji kuwandeleza washiriki. Kila mwalimu anapaswa kuwa na juhudi za kuendeleza ujuzi wa huduma ya washiriki. Mbinu zilizoelezwa katika katika sura hii zitafaa kuwasaidia washiriki kuanza kuzumza katika makundi.