Darasa
Mwalimu anapaswa kupanga darasa mapema kama inawezekana. Washiriki wanapaswa kukaa kwa kutazamana. Mwalimu anapaswa kuhakikisha kwamba kuna nafasi ya kutosha na kuna hakuna vitu ambavyo vitaondoa usikivu na makelele wakati wa somo. Mwalimu anapaswa kujitahidi kuhakikisha kuwa kutakuwa na mkao wa kuridhisha, hewa ya kuridhisha na mwanga wa kutosha. Kusomea nje kunaweza kuwa kuzuri endapo hakuna shughuli za kuharibu usikivu.
Darasa linapaswa kuwa na ubao mkubwa wa kuandikia na kuchorea.
