Kitabu Cha Taasisi Za Wenyeji
Kitabu Cha Taasisi Za Wenyeji
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 5: Mbinu za Ufundishaji Mzuri

4 min read

by Stephen Gibson


Mtindo wa kukaa Darasani

Mwanzoni mwa mafunzo, kuna msisimuko na matarajio. Washiriki hawajui vizuri ni nini cha kutarajia, lakini wana matumaini ya kupata msaada kutoka kwenye kikundi.

Kipindi cha kwanza kinaweza kuwa tofauti na vipindi vingine kwa sababu utatoa utangulizi na ufafanuzi kuhusu darasa ambavyo ni vya lazima. Walakini, kipindi cha kwanza kitaweka mtindo wa vipindi vingine vya baadaye. Kwa mfano, kama mshiriki fulani hatazungumza katika kipindi cha kwanza, mshiriki huyo atatarajia kuwa kimya baadaye. Kama mshiriki mwingine atakuwa anatawala mjadala, kundi litatarajia mijadala ijayo kutawaliwa na mtu yule yule. Kama darasa litakuwa shaghalabaghala, watatarajia hivyo hivyo katika vipindi vingine. Kama darasa lina ushirikishwaji mdogo wa washiriki, watatarajia mfano ule ule.

Baadhi ya washiriki wanaweza kuacha baada ya muda kwa sababu darasa halijawa kama walivyo tarajia. Darasa haliwezi kupangwa kumpendeza kila mtu, lakini linapaswa kuwa lenye kuwaridhisha washiriki wanaotaka kujifunza. Ni muhimu kuliongoza darasa vizuri ili wanafunzi wanaotarajia mambo mazuri wasikate tamaa.