Kitabu Cha Taasisi Za Wenyeji
Kitabu Cha Taasisi Za Wenyeji
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 3: Sifa ya Mwalimu Mtarajiwa

4 min read

by Stephen Gibson


Huduma Maalumu

Walimu ni watu maalumu. Mtume Yakobo anatuonya kwamba sio kila mtu anaweza kuwa mwalimu, kwa sababu walimu wana uwajibikaji wa ki-pekee mbele ya Mungu na watahukumiwa ikiwa hawatakuwa waaminifu (Yakobo 3:1).

Mtume Paulo anaonya kwamba mtu anaweza kujivunia maarifa na kudharau wengine (1 Wakorintho 8:1). Alisema upendo hutusukuma kuwajenga wengine na sio kujiinua wenyewe. Watu wenye maarifa wanapaswa kutambua kuwa maarifa hayo ni zana kwa ajili ya kusaidia wengine na wala sio kitu cha kuwafanya wajione bora. Kama wanatafuta heshima kupitia maarifa, watakuwa na msukumo mbaya na watasababisha madhara.

Maonyo hay ani muhimu kwa watu wanaotaka kufundisha au kutumika katika jukumu lolote la huduma, kwa sababu wanapaswa kusukumwa kujifunza ili kutumika pamoja na maarifa yao.