Kwa kuwa masomo ya SGC yana makusudi ya mafunzo ya huduma, washiriki wanapaswa kuwa waamini wa kikristo walio na ushuhuda mzuri na maisha yanayoheshimika. Asiyeamini hataelewa au hatayathamini yale yaliyoko katika masomo.
Washiriki wanapaswa kuamini misingi ya imani ya kikristo katika ukristo wa asili, ikijumuisha itikadi ya kievangeliko. Masomo yamepangiliwa kutumikia mwili wa Kristo kila mahali, hivyo imani za kimadhehebu hazihitajiki.
Mshiriki anapaswa kuwa mshirika wa kanisa ambaye hushiriki katika ibada na ushirika wa kanisa lake. Washiriki ambao hawako tayari kuheshimu makanisa yao hawatakuwa wajumbe wazuri wa mafunzo. Wanatakiwa kuwa sehemu ya makanisa ambayo yatawaruhusu kuyatendea kazi yale wanayojifunza. Baadhi ya mazoezi yatahusisha ushirikishaji wa waamini wengine.
Taasisi ya wenyeji inapaswa kutumikia washiriki ambao wanaweza kusoman na kuandika vizuri. Sio lazima wawe wahitimu wa masomo ya shule, lakini lazima wajue kusoma na kuandika ili waelewe masomo na kumaliza mazoezi wanayopewa. Taasisi inapaswa kutoa cheti kwa washiriki ambao wanaweza kusoma katika kiwango hiki.
Viwango vingine vya mafunzo vinaweza kutolewa kwa washiriki ambao wanataka kujifunza lakini hawana uwezo wa kufanya mazoezi wanayopewa. Kwa mfano, walimu wanaweza kufundisha kusanyiko kubwa au kikundi cha kujifunza Biblia kukiwa na watu ambao hawajui kusoma vizuri na hawawezi kufanya mazoezi wanayopewa.
Kuwaelewa Washiriki Wetu
Washiriki ambao wanaandikishwa katika SGC wako tofauti na wanafunzi wa aina za taasisi zingine. Hawa sio sawa na watoto wa shule. Wako tofauti na wanafunzi wa vyuo vikuu na tofauti na wanafunzi wengi wa vuuo vya Biblia. Walimu wanalazimika kubadili mbinu za kufundisha katika aina ya darasa la namna hii. Uwezo wa kielimu wa baadhi ya washiriki utakuwa mdogo kuliko uwezo wa mwanafunzi wa chuo. Walimu ni lazima warekebishe matazamio yao. Wanapaswa kufafanua ni namna gani washiriki wanatakiwa kufanya mazoezi yao. Wanapaswa kukemea uvivu na uzembe, lakini uchambuzi wao kwenye mazoezi ya washiriki unapaswa kuwa wa kujenga, kutia moyo, na usioonyesha dharau.
Kumbuka, kama Mungu amewaita watu katika huduma, Mungu ndiye anawapa uwezo wanaouhitaji. Washiriki wanaweza kuwa wameshaonyesha upako na baraka za Mungu katika huduma zao. Ni wajibu wetu kuwasaidia kuwakuza. Itakuwa ni makosa kuwakatisha tamaa.
Kutakuwa na tofauti ya miaka kati ya makundi ya washiriki wa SGC. Baadhi yao wanaweza kuwa wamemaliza shule karibuni. Wengine wanaweza kuwa na umri wa kutosha kuwa babu. Labda wengine wamekuwa wachungaji kwa miaka mingi. Wakati mwingine mshiriki anaweza kuwa na umri mkubwa kuliko mwalimu.
Mshiriki mwenye umri wa miaka ishirini aliyemaliza shule anaweza kuwa na uwezo mkubwa wa kitaaluma kuliko mchungaji ambaye ana umri wa miaka sitini. Hata hivyo, kila mtu anapaswa kupewa heshima. Tunapaswa kutoheshimu uwezo wa kielimu kwa namna ambayo inawakosea adabu wenye ukomavu na uzoefu. Tukiwa tunasisitiza matakwa ya kielimu, tunapaswa kuepuka kuwaibisha washiriki ambao hawajapitia mafunzo kama hayo.
Tabia za Watu wazima wanaojifunza
Neno hili la mwanafunzi mtu mzima hutumika kumwelezea mshiriki ambaye ameshaanza maisha ya utu uzima. Watu wazima wanaojifunza wanaweza kuwa wameoa au kuolewa na wana Watoto. Wanaweza kuwa wanafanya kazi za kulipwa au huduma. Tayari hawa wana uzoefu tofauti tofauti. Pale ambapo mtu mzima anachagua kuwa mwanafunzi tena, wanakuwa wanataka kufikia malengo fulani.
Mtindo wa mwalimu na darasa vinapaswa kuwekwa kwa namna ambayo watu wazima wajifunzao wanahitaji.
Watu wazima wanaojifunza wanataka mafunzo ambayo yatawasaidia haraka. Wanataka kujadiliana jinsi ya kufanya kwa vitendo yale ambayo wanajifunza. Darasa linapaswa kuwapa washiriki muda wa kuelezea jinsi wanavyotarajia kutumia maarifa hayo. Mwalimu hapaswi kutumia muda wote wa darasa kwa kuwasilisha mada bila kujadiliana na washiriki.
Watu wazima wanaojifunza wanataka heshima. Tayari wana majukumu ya utu uzima na hawataki kufanyiwa kama watoto. Walimu wanapaswa kuwa na mtazamo wa kujifunza kupitia wengine na kuwa tayari kupokea jambo jipya tofauti na lao. Wanapaswa kuonyesha heshima kwa uzoefu na maarifa ya washiriki wao.
Watu wazima wanaojifunza wanataka kufanya chaguzi wanaposoma. Uzoefu wao na malengo yao vinafanya aina fulani ya kujifunza inayowavutia na inayowafaa wao. Wanahitaji uhuru kufuata matarajio yao na kuendeleza mtindo wao wa kujifunza.
Watu wazima wanaojifunza hutaka kufanya mazoezi ya vitendo darasani. Mwalimu anapaswa kuwafanya washiriki kuwasilisha mijadala yao darasani, wakielezea sehemu ya mada, na kuwasaidia kujibu maswali. Wakati mwingine washiriki wanaweza kusimulia visa walivyokutana navyo katika uzoefu wao wa maisha. Ingawa walimu ni lazima waepuke kupoteza muda, wanapaswa vilevile kufahamu kwamba simulizi inaweza kuwa njia ya mshiriki kutumia katika Maisha yake kitu alichojifunza.
Watu wazima wanaojifunza wanajenga mahusiano na washiriki wenzao. Hujifunza kutokana na mirejesho ya wenzao. Hutoa na kupokea heshima. Watu wazima wanaojifunza watakumbuka na kuthamini maishani mambo kadhaa waliyojadiliana. Darasa kwa nyakati tofauti linahitaji kugawanyika katika vikundi vidogo ili wafanye mijadala.
Watu wazima wanaojifunza hutaka kukata shauri. Wanategemea maoni tofauti kuvumiliwa.
Watu wazima wanaojifunza wanataka kumpenda na kumheshimu mwalimu. Hawategemei kuona hadhi tofauti kati yao na mwalimu kama vile tofauti ilivyo kati ya wanafunzi na profesa katika vyuo vikuu. Wanathamini kusikilizwa binafsi na mwalimu. Wanatamani sio maarifa tu lakini pia na uwajibikaji na tabia ya mwalimu.
Mrejesho kwa Mshiriki
Mwalimu anapaswa kupata muda wa kutosha darasani na kwa mshiriki mmoja mmoja kuzungumzia mazoea mazuri ya kusoma. Washiriki wanapaswa kujifunza jinsi ya kujidhibiti na kufuata ratiba ya kusoma kila siku.
Mwalimu anapaswa kutunza kumbukumbu za mazoezi na mahudhurio ya washiriki vizuri. Mwishoni mwa somo, kumbukumbu hizo zitatumika kwa kutoa alama za somo. Wakati wa somo, ambapo washiriki binafsi hawafanyi vizuri, mwalimu anapaswa kuzungumza nao na kuwaeleza jinsi ya kuboresha.
Ni muhimu kwa mwalimu kuhakikisha mwanafunzi anaelewa jinsi ya kufanya mazoezi. Mazoezi yafanywayo vibaya yanapaswa kurudishwa kwa mshiriki ili kufanya masahihisho, lakini mwalimu anapaswa kuhakikisha kwamba mshiriki anaelewa jinsi ya kusahihisha kazi yake.
Kama mahudhurio ya washiriki au mazoezi yao yanafanya alama za somo kuwa chini, mwalimu anapaswa kuzungumza nao kuhusu hitaji la kuboresha. Kwa hali hiyo washiriki hawatashangazwa na alama za matokeo yao mwishoni mwa somo.
SGC exists to equip rising Christian leaders around the world by providing free, high-quality theological resources. We gladly grant permission for you to print and distribute our courses under these simple guidelines:
No Changes – Course content must not be altered in any way.
No Profit Sales – Printed copies may not be sold for profit.
Free Use for Ministry – Churches, schools, and other training ministries may freely print and distribute copies—even if they charge tuition.
No Unauthorized Translations – Please contact us before translating any course into another language.
All materials remain the copyrighted property of Shepherds Global Classroom. We simply ask that you honor the integrity of the content and mission.