Kitabu Cha Taasisi Za Wenyeji
Kitabu Cha Taasisi Za Wenyeji
Audio Course Purchase

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 4: Kuwaelewa Washiriki Wetu

5 min read

by Stephen Gibson


Sifa za kidini

Kwa kuwa masomo ya SGC yana makusudi ya mafunzo ya huduma, washiriki wanapaswa kuwa waamini wa kikristo walio na ushuhuda mzuri na maisha yanayoheshimika. Asiyeamini hataelewa au hatayathamini yale yaliyoko katika masomo.

Washiriki wanapaswa kuamini misingi ya imani ya kikristo katika ukristo wa asili, ikijumuisha itikadi ya kievangeliko. Masomo yamepangiliwa kutumikia mwili wa Kristo kila mahali, hivyo imani za kimadhehebu hazihitajiki.

Mshiriki anapaswa kuwa mshirika wa kanisa ambaye hushiriki katika ibada na ushirika wa kanisa lake. Washiriki ambao hawako tayari kuheshimu makanisa yao hawatakuwa wajumbe wazuri wa mafunzo. Wanatakiwa kuwa sehemu ya makanisa ambayo yatawaruhusu kuyatendea kazi yale wanayojifunza. Baadhi ya mazoezi yatahusisha ushirikishaji wa waamini wengine.