Huduma Ya Uongozi

Huduma Ya Uongozi

Utangulizi

Kikundi cha vijana kinacheza kwa pamoja. Yohana anasema, “Nyie, tucheze mpira.” Inaonekana hakuna anayeonyesha kuwa na taarifa kwamba Yohana amezungumza. Kisha Thomasi akasema, “George, nenda ukalete ile miti, na tutacheza kama sisi ni wanajeshi.” George akaenda kuchukua ile miti, na wale vijana wakaanza kujipanga kucheza kana kwamba wao ni jeshi.

► Je, ni nani kiongozi katika kikundi hiki, Yohana au Thomasi? Kiongozi ni nani? Kwa nini tunaweza kusema kwamba uongozi siyo lazima umaanishe ni nafasi ya mamlaka?