Warumi
Kitabu cha masuala mengi yaliyofanyiwa Mjadala
Mambo mengi ya kiteolojia yamefanyiwa mijadala katika kanisa kwa karne nyingi zilizopita. Kitabu cha Warumi kinashughulika na masuala tata ya kiteolojia labda kuliko kitabu kingine chochote cha Biblia. Hapa kuna mifano ya maswali yaliyopata majibu katika barua hii.
Maswali ya kiteolojia yaliyopata majibu katika kitabu cha Warumi
Angalizo kwa kiongozi wa darasa: Somo kila swali na toa nafasi ili kuruhusu wanafunzi kadhaa waweze kutoa majibu. Kikundi hakipaswi kitumie muda wake mrefu kwenye kujibu swali lolote na hakipaswi kijaribu kufikia kwenye hitimisho. Kusudi la orodha hii ya maswali ni kuonesha kwamba kuna maoni mengi kuhusiana na maswali haya.
1. Je, mtu anapaswa aamini kitu gani ili aweze kuokoka kwa njia ya imani?
2. Je, inamaana gani kwamba Mkristo hawezi kuupata wokovu wake kwa njia ya njia ya matendo?
3. Je, Mungu aliamua kuokoa baadhi ya watu, na akaamua kuwaacha wengine?
4. Je, ni kwa jinsi gani Mungu anachagua mtu aliyeokoka na ambaye hajaokoka.
5. Je, ni jambo gani litakalotokea kwa watu ambao kamwe hawajawahi kuisikia injili?
6. Je, ni kwa jinsi gani Mungu anaweza kuwa mwenye haki kama anasamehe baadhi ya watenda dhambi na wengine kuwaadhibu?
7. Je, mtu aliyeamini ataweza kuwa bado mwenye dhambi?
8. Je, ni ushindi gani wa kiroho unaowezekana kwa ajili ya maisha halisi?
9. Je, kuna uwezekano kwa mtu aliyeokoka kupoteza wokovu?
10. Je, Mungu bado anao mpango kwa ajili ya Israeli?
Please select a section from the sidebar.