Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa

Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa

Utangulizi

► Kwa nini unaenda Kanisani?

Wakati watu wanapozungumzia kuhusu “kwenda kanisani” wanamaanisha kwenda kwenye nyumba ya ibada kwa ajili ya ibada iliyopangwa.

Watu wengi Wanasema wanatenda kanisani kwa ajili ya kujifunza kuhusu Mungu. Watu wengine wanaojisikia wako mbali na Mungu huenda kanisani wakitegemea kuusikia uwepo wa Mungu. Watu wanaomjua Mungu huenda kanisani wakitegemea kuusikia na kuupata uwepo wake Mungu kwenye sifa. Kanisa ni kuhusiana na Mungu. Watu wanapaswa waweze kuusikia na kupata uwepo wa Mungu kwenye ibada za kumsifu Mungu za kanisa.

Lakini kanisa siyo jengo, na vile vile siyo mahali pa makutaniko ya kusifu. Kanisa ni kusanyiko la waumini ambao wamedhamiria kwa pamoja kuwa kanisa. Kwa hiyo, Tunaposema kuhusu watu kuliona kanisa au kwenda kanisani, tunamaanisha ni kikundi cha watu walioamini. Tunaposema kwamba kanisa ni kuhusiana na Mungu, hatumaanishi tu kwamba jengo na ibada ya kusifu ni kuhusiana na Mungu. Maisha ya kikundi cha watu waliodhamiria waliyo nayo kwa pamoja ndiyo kuhusiana na Mungu.